KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, August 28, 2012

EABL KUPITIA TUSKER LAGER WATOA DOLA 450,000 KUDHAMINI TUSKER CUP.

Captions: DSC 5445: Uganda Breweries Marketing Director Lemmy Mutahi  (C ) handing over a dammy cheque to Cecafa General Secretary Nicholas Musonye. Extreem right is FUFA Vice President Livingstone Kyambadde in Kampala on Tuesday.

DSC 5503: Cecafa General Secretary Nicholas Musonye receives a this year's Cecafa-Tusker cup from EABL (U) Marketing Director Lemmy Mutahi at Serena Hotel Kampala on Tuesday. On the right is FUFA Vice President Livingstone Kyambadde.

Cecafa General Secretary Nicholas Musonye chats with the Cecafa Founder Member Kezekia Ssegwanga Musisi before the official launch of this year's Cecafa-Tusjker Cup 2012 at serena Hotel Kampala Tuesday.

Tusker Lager,ambao ni miongoni mwa wadhamini wakubwa wa michezo katika ukanda wa Afrika mashariki na kati jumanne hii wametangaza udhamni wao wenye thamani ya dolari za kimarekani  USD 450,000 kwa ajili ya michuano ya Tusker Cup ambayo imepangwa kufanyika katika jiji la Kampala nchini Uganda.
Baraza la vyama vya soka Afrika Mashariki na kati (CECAFA) limetangaza kuwa michuano hiyo itafungua pazia November 24 katika uwanja wa taifa wa Mandela ,Namboole.
Michuano hiyo itafikia kikomo December 8.Katibu wa Nicholas Musonye ambaye alielekea Kampala jana kwa ajili ya kuhudhuria kikao cha maandalizi ya michuano hiyo.
Wakifungua udhamini wao huo hapo jana katika Hoteli ya Serena jijini  Kampala, Mkurugenzi wa masoko wa kampuni ya bia EABL Lemmy Mutahi amesema uamuzi umekuja kujaribu kuzisaidia timu za mataifa ya Afrika Mashariki kwa ajili ya safari ya kuelekea kwenye fainali ya Kombe la dunia 2014.
Amesema wadhamni wamefurahia michuano hiyo kupelekwa nchini Uganda ambapo kwa mwaka huu wameongeza sehemu ya udhamni wao kwa asilimia 5% ukilinganisha na mwaka jana.
Kwa upande wake Musonye amesema udhamini huo utakuwa ni pamoja na mambo mengine ni  malazi na usafiri wa ndege kwa timu shiriki. Kiasi cha dolari za Kimarekani USD 60.000 zitakuwa ni zawadi ambapo mshindi atazawadiwa dolari  USD 30.000, na mshindi wa pili USD 20.000 wakati ambapo mshindi wa tatu atapata dolari za kimarekani USD 10.000
Musonye amesema pia michezo yote itaonyeshwa na kituo cha television cha Super Sport.

No comments:

Post a Comment