KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, August 28, 2012

MAPINGAMIZI YAZIDI KUONGEZEKA, DAVID LUHENDE NAYE YUMO SOMA BAADHI YA MAJINA.


Wakati kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji chini ya Mwenyekiti wake Alex Mgongolwa ikitarajia kukutana Jumapili (Septemba 2 mwaka huu) kupitia usajili wa wachezaji kwa msimu wa 2012/2013, taarifa zinasema kumejitokeza idadi kubwa ya mapingamizi ambao watajadiliwa katika kikao hicho.

Usajili utakaopitiwa ni wa klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Lidi Daraja la Kwanza (FDL) ambapo Kamati itapitia pingamizi zilizowasilishwa na klabu mbalimbali dhidi ya wachezaji waliosajiliwa na klabu zingine.

Mbali na mapingamizi ya akina Kelvin Yondani Mbuyu Twite na Ramadhani Chombo Lidondo mapingamizi mengine mengi yamejitokeza toka kwa vilabu mbalimbali.

 Miongoni mwa vilabu vilivyo weka pingamizi ni pamoja na Kagera Sugar ambayo inapinga David Luhende kwenda Yanga kwa vile hajafanyiwa uhamisho. Flamingo ya Arusha inapinga wachezaji wake Kelvin Friday Idd kwenda Azam na Salim Walii kwenda Polisi Mara kwa vile hawajafanyiwa uhamisho. Toto Africans inapinga wachezaji wake Enyinna Darlinton kwenda Kagera Sugar na Mohamed Soud kwenda Coastal Union kwa vile bado ina mikataba nao. Hao ni baadhi tu ya wanaopingwa, lakini wako wengi.

No comments:

Post a Comment