Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza rasmi Mart Nooij kutoka Uholanzi kuwa
kocha mkuu mpya wa timu ya Taifa (Taifa Stars).
Rais
wa TFF, Jamal Malinzi amemtambulisha kocha huyo leo (Aprili 26 mwaka huu) kwenye
mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Akiwa
amefuatana na Makamu wake Wallace Karia, amesema anafurahi kumtangaza Nooij na
ana matarajio kuwa Tanzania itanufaika na uzoefu wake mkubwa wa ukocha, hasa
katika bara la Afrika.
“Nawaahidi
Watanzania kuwa sitomuingilia kocha katika kazi yake. Kama mimi sitomuingilia
kocha, basi hakuna mtu yeyote atakayemuingilia. Tumemwajiri yeye kwa vile ni
mtaalamu, hivyo hakuna sababu ya kumuingilia,” amesema Rais Malinzi.
Naye
Nooij ambaye amepewa mkataba wa miaka miwili amesema yeye ni mtu wa maneno
mafupi, hawezi kuahidi kitu lakini ana matarajio ya kuifanya Taifa Stars ifanye
vizuri katika mashindano mbalimbali.
Amesema
kabla ya kukubalia kufundisha Taifa Stars alikuwa na klabu ya St. Georges ya
Ethiopia, lakini vilevile amewahi kufundisha mpira wa miguu barani Afrika
katika nchi za Burkina Faso, Mali na Msumbiji.
Wasifu wake
Nooij amewahi kuwa kuwa mkufunzi wa maendeleo katika chama cha soka nchini Uholanzi kabla ya kuanza kuafanya kazi katika kituo cha EVC 1913 katika nchi za Marekani na Kazakhstan. Amekuwa pia meneja wa timu ya vijana ya Bukina Faso ya wachezaji wenye umri chini ya miaka 20 katika fainali za kombe la dunia la vijana la Fifa mwaka 2003.
Mwka 2007 aliteuliwa kuwa kocha wa timu ya taifa ya Msumbiji na akiwa kama meneja aliiwezesha nchi hiyo kufuzu kucheza fainali za mataifa ya Afrika 2010 baada ya kipindi cha miaka 12 kupita.
Kufuatia kushindwa kufuzu kwa fainali zilizofuata mwaka 2012 Nooij alijiuzulu kazi hiyo Septemba mwaka 201.
Mnamo April 19 April 2012, alichukuliwa na Santos ya Afrika kusini inayoshiriki ligi kuu ya nchini Afrika Kusini, lakini alifukuzwa kazi desemba 18 2012.
November 2013, Nooij akaajiriwa na Saint George ya Ethiopia na miezi mitano iliyofuatia yaani April 25 akakubali kazi ya ya kuifundisha timu ya taifa ya Tanzania.
No comments:
Post a Comment