KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, May 11, 2014

Mdudu wa ushoga nchini Marekani aingia katika mchezo wa NFL. Bonge la mtu Michael Sam naye shoga

Mchezaji mmoja wa timu ya ligi ya soka ya Marekani, National Footbal League ,Michael Sam amekuwa mchezaji wa kwanza kutangaza wazi kwamba yeye ni shoga katika mchezo huo.
Sam alikuwa ameteuliwa na timu ya Saint Louis Rams katika siku ya mwisho ya usakaji wa vipaji katika mchezo huo ulio maarufu zaidi nchini marekani.
Hatua hiyo ya Michael Sam kutangaza jinsia yake mnamo mwezi february baada ya kukamilisha masomo yake ya mchezo huo katika chuo cha Missouri ilipongezwa ,huku rais Obama akiwa miongoni mwa watu waliotoa pongezi zao.
Baadhi ya wachambuzi wa michezo walikuwa wamebashiri kwamba baadhi ya timu huenda zikajitenga na umaarufu unaomzunguka mchezaji huyo.

No comments:

Post a Comment