KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, May 5, 2014

Nyasi Bandia: Uwanja wa Kaitaba nao umo, wakaguliwa kabla ya Nyamagana Mwanza kufuatia kesho

Majukwaa ya uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba

Mtaalamu wa nyasi bandia kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Ian McClemen leo wameanza kukagua ukaguzi wa uwanja wa mpira wa miguu wa Kaitaba mjini Bukoba kablan ya hapo kesho kukagua Uwanja wa Nyamagana tayari kwa maandalizi ya kazi ya uwekaji wa nyasi za bandia.

Viwanja hivyo vinawekwa nyasi bandia kwa ufadhili wa shirikisho la soka duniani FIFA chini ya mpango wa misaada wa Goal Projects.

 Baada ya ukaguzi huo, McClemen atatuma ripoti yake FIFA ili shirikisho hilo liweze kuteua mkandarasi wa kufanya kazi hiyo.

Uwanja wa Kaitaba ni miongoni mwa viwanja ambavyo vilivyofungiwa na TFF baada ya nusu msimu wa ligi kuu ya soka Tanzania bara huku amri ya marekebisho ikitolewa kabla ya kuanza duru ya pili la ligi hiyo.

Uwanja huo ulisimamishwa kutokana na majukwaa yake kuchakaa, hivyo kuhatarisha usalama wa watazamaji.

 Kwa upande wa uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza wenyewe ulikuwa katika mpango huo wa FIFA wa Goal Project 4 tangu awali ambapo kiasi cha dola 630,000 (zaidi ya Sh bilioni moja) kimepangwa kutumika katika kuukarabati uwanja huo mkongwe wa soka kwa lengo la kuufanya uwe wa kisasa.

Ukarabati huo utajumuisha uwekwaji wa nyasi bandia pamoja na taa kwa ajili ya matumizi ya uwanja huo nyakati za usiku.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Evarist Ndikilo alisema uwanja huo unatarajiwa kufanyiwa ukarabati mkubwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) limetoa dola 500,000 kwa ajili ya kazi hiyo, huku Halmashauri ya Jiji la Mwanza ikiridhia kuongeza kiasi kingine cha dola 130,000 kwa ajili ya kuuboresha kwa kuuwekea taa, viti na nyasi bandia.

Kwa Tanzania viwanja vilivyowekwa nyasi bandia hadi sasa kupitia Goal Project ni Uwanja wa Uhuru uliopo Dar es Salaam, Uwanja wa Karume (Dar es Salaam) na Uwanja wa Gombani uliopo Pemba.
Hii ndio sura ya uwanja wa Nyamagana kwa sasa

No comments:

Post a Comment