Kocha mkuu wa Simba Milovan Cirkovic |
Kocha wa
Simba Milovan Circovich amewatoa wasiwasi wapenzi na mashabiki wa klabu hiyo
katika changamoto ya kusaka taji la michuano ya Kagame huku akisema wamekuwa
wakiendelea na mazoezi vizuri na Simba ipo tayari ajili ya mchezo wa kesho
dhidi ya Vita club ya DRC.
Circovich licha
ya kwamba mchezo wa kesho kutokuwa na umuhimu wowote kwao kwakuwa timu hiyo
imeshaingia katika hatua ya robo fainali ya michuano hiyo bado watahitaji
ushindi .
Amesema
kimsingi timu ipo katika hali nzuri licha ya kukabiliwa na pengo mlinzi wa
kushoto Amir Maftaha ambaye amepata matatizo katika kidole cha mkononi lakini
kocha huyo amesema pengo lake litazibwa na Kigi Makasi.
Shomari Kapombe alikuwa na maumivu kidogo lakini
Circovich amesema kwasasa anaendelea vizuri na amezungumza naye ameonyesha kuwa
yuko fiti na tayari kwa ajili ya mchezo wa kesho lakini ameshindwa kuthibitisha
kama atamtumia ama hapana.
Akizungumzia
kikosi cha Vita club ya DRC kocha huyo wa Simba amesema anajua kuwa Vita ni
timu nzuri lakini haiogope na waanamini wamejiandaa vizuri na hawaihofii timu
yoyote kwenye kagame.
Amesema
Simba kwasasa ina pengo la Emmanuel Okwi ambalo limeathiri sana sehemu ya
ushambuliaji lakini katika kuhakikisha anafanikiwa kuziba pengo hilo kwasasa
anamtengeneza Abdalah Juma ili aweze kuliziba pengo hilo.
Amewataka
mashabiki wa Simba kuwa na subira katika kipindi hiki ambacho kocha anajaribu
kutengeneza timu kwasababu wameondokewa na wachezaji muhimu kama Patrick Mafisango
aliyefariki dunia May 16 na Emmanuel Okwi aliyekwenda kujaribu kucheza soka barani ulaya.
No comments:
Post a Comment