KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, August 2, 2012

SOMA HABARI ZA KIMICHEZO KIMATAIFA.Inter yapata wamiliki wa bara Asia,Busquets azungumzia juu ya ubora wa Song na nyingine nyingi.

Sturridge anataka kucheza kama mshambuliaji wa kati Chelsea 2012-13
mshambuliaji wa Chelsea Daniel Sturridge ameweka wazi juu ya nia yake ya kucheza sehemu ya ushambuaji wa kati katika klabu yake msimu ujao kufuatia kuondoka kwa Didier Drogba.
mshambuliaji huyo kwasasa yuko katika timu ya GB katika michuano ya Olympics, na alikuwa akitumika sehemu ya kiungo wa pembeni katika msimu wa 2011-12 mna kufunga jumla ya mabao 13 katika michuano yote
amenukuli wa akiongea na talkSPORT akisema
"nimekuwa nikisubiri fursa hiyo ya kushambulia toka kati tangu najiunga na Chelsea na nina matumaini msimu nityakuwa ni miongoni mwa wachezaji wa kati ambapo nitaonyesha uwezo wangu nina imani meneja atanipa nafasi. "
mchezaji huyo wa zamani wa City player kwasasa anakabiliwa na ushindan I mkubwa katika sehemu ya ushambuliaji kufuati katika majira haya ya usajili klabu hiyo kumuongeza Marko Marin, Eden Hazard na kaka yake Thorgan, lakini anasema anafurahia mabingwa hao wa soka ulaya kuongezxa nguvu kikosini.
Giroud:Nashawishika Arsenal itakuwa moto
mshambuliaji wa washika mitutu wa Arsenal Olivier Giroud anamatumaini kuwa timu yake mpya itawashangaza watu msimu itakapo twaa taji.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 25 hakuwashanga watu kuongezwa katika kikosi hicho baada ya kuisaidia Montpellier katika ligi ya soka nchini Ufaransa ya msimu uliopita.
Giroud alimaliza msimu aliungana na mshambuliaji wa PSG  Nene kuwa wafungaji bora wakifunga jumla ya mabao 21 kila mmoja lakini pia akipiga pasi za mwisho zilizo zaa magoli tisa lakini pia akitoa msaada katika timu yake ya taifa ya Ufaransa katika michuano ya Euro 2012.
amenukuliwa akisema aliona mambo mengi yenye kufanana kati ya Arsenal na Montpellier jambo ambalo limekuwa ni sababu kubwa ya kukubali kujiunga na klabu hiyo toka pande za kasakazini mwa jiji la London.
Chelsea yathibitisha kumtoa De Bruyne
Chelsea imethibitisha kuwa Kevin De Bruyne amejiunga na Werder Bremen kwa mkopo wa muda mrefu.
De Bruyne mwenye umri wa miaka 21 alijiunga na Chelsea mwezi January kwa ada ya pauni ya milioni £6.7 lakini alikopeshwa kwa Genk mpaka kumalizika kwa msimu.
Nyota huyo wa kimataifa wa Belgium alikuwa katika mazoezi na Blues majira haya ya kiangazi lakini klabu hiyo imeamua kumkopesha tena kwa lengo la kumuongezea uzoefu zaidi.
taarifa katika mtandao wa klabu hiyo imesema
"winga huyu sasa ataendelea kujenga uwezo katika  Bundesliga sehemu ambayo anategemea kupata nafasi ya kuchukua nafasi ya Marko Marin."
De Bruyne anatazamiwa kupata mafanikio katika klabu ya Werder Bremen.
Busquets azungumzia juu ya ubora wa Song

kiungo wa Barcelona Sergio Busquets amesema angependelea kuona kiungo wa Arsenal Alex Song akijunga na Catalan.
Kuondoka kwa Seydou Keita kuelekea katika klabu moja huko uchina ya Dalian Aerbin mapema majira haya ya kiangazi kumeacha pengo katika sehemu ya kiungo na Busquets anaamini  Song ambaye mkataba wake na Arsenal unatarajiwa kumalizika mwaka 2014 atakuwa amepeleka ushindani mkubwa katika kikosi chao.
amenukuliwa akisema
"Song ni mchezaji mzuri sana anajituma na ananguvu" "yuko kijana toka Barca B Sergi Roberto anaandaliwa lakini nadhani ni vizuri kuwa na chaguo lingine toka ndani.
Busquets amerejea katika mazoezi wiki hii baada ya kutoa msaada katika timu taifa ya Hispania katiika Euro 2012.
Kikosi cha Barca kitaungana tena hapo kesho huku Jordi Alba, Cristian Tello na Martin Montoya wakirejea toka katika michuano ya Olympic mapema kuliko ilivyo tarajiwa.
Barcelona inaendelea na michezo yao ya maandalizi ya msimu na jumamosi watakuwa na mchezo dhidi ya timu iliyofanya usajili wa mapesa mengi msimu huu Paris St-Germain.

Wachezaji watimuliwa mashindanoni
Timu ya mpira wa miguu ya Uswizi imemfukuza beki wake Michel Morganella kutoka mashindanoni kwa kutuma ujumbe wa ki-ubaguzi wa rangi akitumia mtandao wa Twitter.
Mchezaji huyo alituma ujumbe ukiwalenga watu wa Korea ya kusini kwa ujumla kupitia Twitter baada ya Timu yake kupoteza mechi dhidi ya Korea ya kusini 2-1 jumapili iliyopita.
Tangu hapo mtandao huo umefutwa na beki huyo kuomba radhi, akisema kweli, nilikosea sana baada ya matokeo yasiyoridhisha, alisema kijana huyo mwenye umri wa miaka 23.

Morganella aliongezea kusema kua: "ningependa kuwaomba radhi raia wote wa Korea ya kusini na timu yao, vilevile ujumbe wa Uswizi na mchezo wa mpira kwa ujumla nchini Uswizi."
Mapema mwezi huu, mwanariadha wa Ugiriki wa kuruka hatua tatu kuelekea mchangani Paraskevi Papachristou alitimuliwa kutoka kwenye kikosi cha Olimpiki cha nchi yake kufuatia matamshi aliyoyatoa kupitia Twitter yaliyoonekana kuwa ya kiubaguzi wa rangi.
Kocha mkuu wa Kikosi cha Uswizi Gian Gilli alisema kua Morganella, anayecheza soka yake ya kulipwa na klabu ya Italia -Palermo ameidhalilisha timu nzima. Kocha huyo amesema kua alibagua, katukana na kukiuka hadhi ya raia na wachezaji wa timu nzima ya Korea ya kusini.
Inter yapata wamiliki wa bara Asia

Klabu ya Uitaliano Inter Milan inasema kua kundi la wawekezaji kutoka Uchina limejitokeza kua wawekezaji wa pili kwa ukubwa wa kumiliki hisa za klabu hiyo.
Katika taarifa ya Internazionale Holding,kampuni mama inayosimamia masuala yote yanayohusiana na klabu imesema kua kundi hilo limetangaza kua litamiliki sehemu ya hisa lakini kwamba familia ya Moratti itaendelea kumiliki sehmu kubwa ya biashara.
Taarifa hio imesema kua uwanja mpya utajengwa chini ya ushirikiano na sehemu ya China Railway Construction ikitazamiwa kukamilishwa mnamo mwaka 2017.
Klabu hio imetangaza kua Kamchi Li, Kenneth Huang na Fabrizio Rindi wote watakua wakurugenzi kwenye bodi kutokana na uwekezaji huu.
Inter ndio klabu ya hivi karubini kuvutia wawekezaji kutoka barani Asia. Klabu ya jijini London na Ligi kuu ya Premiership Queen's Park Rangers ina milikiwa na Tony Fernandes, huyu akiwa mmiliki wa kampuni uya ndege baranoi Asia, Air Asia, baada ya kukamilisha ununuzi wake mwaka jana.

Arsenal kusajili wawili kwa mpigo
Arsenal inajitahidi kukamilisha utiaji saini wa makubaliano ya mkataba wa kudumu na mchezaji Santi Cazorla kutoka klabu ya Malaga pamoja na mcheza kiungo mwenzake Nuri Sahin anayeingia kwa makubalino ya mkopo kutoka klabu ya Real Madrid.
Mpango wa kuhama kwa mchezaji wa Timu ya Taifa ya Uhispania Cazorla mwenye umri wa miaka 27 kumekua na utata wa shida ya fedha inayoikumba klabu ya Malaga hata hivyo anatazamiwa kupitia utaratibu wa afya wiki hii.
Mcheza kiungo wa timu ya Taifa ya Uturuki mwenye umri wa miaka 23 Nuri Sahin atajiunga na Arsenal chini ya mpango wa mkopo wa mwaka mmoja na Real Madrid.
Lililobaki ni baina ya mchezaji Sahin kukubaliana na klabu ya Arsenal juu ya malipo na marupurupu. Kuna uwezekano mkubwa kwa wachezaji hawa kuhitimisha utaratibu huu kabla ya msimu mpya kuanza.
Bado Sahin hajapangiwa siku ya kufanyiwa majaribio ya afya. Arsenal inaanza msimu mpya kwa pambano la ugenini dhidi ya Sunderland mnamo tareh 18 Agosti.
Tayari Gunners imewasajili wachezaji wawili mshambuliaji Lukas Podolski kutoka klabu ya Cologne na mshambuliaji wa Ufaransa Olivier Giroud aliyekuwa akichezea klabu ya Montpellier.
Pamoja na hayo yote wingu zito bado limegubika majaliwa ya nahodha Robin van Persie, ambaye ametamka kua hatoongezea mkataba wake unaomazika mwaka 2013.
Usajili wa wacheza kiungo Cazorla pamoja na Sahin ingawa hakuna uhusiano na mizengwe ya Van Persie lakini umechagizwa na habari kwamba mcheza kiungo wa Arsenal Jack Wilshere hatoweza kucheza kabla ya mwezi oktoba kutokana na jeraha la goti.
Cazorla aliyejiunga na Malaga kutoka klabu ya Villarreal mwaka mmoja tu uliopita ana urefu wa futi 5 inchi 6 na ameichezea timu ya Taifa ya Uhispania mwaka 2008 na kwenye mashindano ya Ulaya ya mwaka 2012.
Sahin alisajiliwa na Real Madrid kutoka Borussia Dortmund kwa mkataba wa miaka sita mnamo mwezi May 2011 lakini ameshindwa kupata nafasi katika kikosi Mourinho ambapo kocha huyo ameweza kumruhusu aondoke tu ila kwa mkopo.

No comments:

Post a Comment