KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, November 27, 2012

JOHN TERRY AJIFARIJI KWA KUVAA JEZI YA DI MATTEO.

 Nahodha wa Chelsea John Terry amemtumia maneno ya faraja na pole meneja wake wa zamani Roberto Di Matteo muda mfupi kabla ya mchezo wa kwanza wa mrithi wake Rafa Benitez dhidi ya Manchester City mchezo uliochezwa jumapili.

Mlinzi huyo yuko kwasasa yuko nje ya uwanja kufuatia maumivu ya mguu.

Mlinzi huyo katika kujifariji na kuonyesha ni namna gani alivyoguswa na kuondolewa kwa Di Matteo Stamford Bridge,  alilazimika kuweka pembeni jezi yake yenye nambari 26 japo kwa muda na kuvalia jezi nambari 16 kabla ya kuingia uwanjani kufanya mazoezi ya viungo na wataalamu wa viungo wa klabu yake.

Jezi hiyo namba 16 ilikuwa ikivaliwa na Di Matteo enzi za uchezaji wake wakati alipokuwa mchezaji wa Chelsea kwa kipindi cha miaka minne.

Hata hivyo licha ya kumuunga mkono meneja wake huyo wa zamani, Terry amesisitiza kuwa ndani ya chumba cha kubadilishia nguo hali ni shwari na vijana wameungana na Benitez licha ya upinzani kutoka katika viunga vya  Merseyside.

"Alhamisi tulimkaribisha Rafa Benitez kama meneja wetu mpya na wachezaji wote wanaangalia mbele kufanya naye kazi"

No comments:

Post a Comment