Zambia imekuwa ni bingwa wa kwanza katika fainali za mataifa ya Afrika kuondolewa katika mzunguko wa kwanza katika kipindi cha miaka 21 ya michuano hiyo baada ya kwenda sare ya bila kufungana na Bukina Faso mchezo wa kundi C wa michuano hiyo inayofanyika nchini Afrika kusini.
Mazingira kama hayo yaliwahi kuwakuta Algeria, ambao walishindwa kutinga hatua kama hiyo mwaka 1992 wakiwa ni mabingwa watetezi.
Wakati Zambia wakishindwa kufanya hivyo, wao Nigeria wamefanikiwa kushika nafasi ya pili katika kundi hilo baada ya kuifunga Ethiopia kwa mabao 2-0 katika mchezo mwingine uliochezwa katika muda unaofanana kuepusha upangaji wa matokeo mjini Rustenburg.
Matokeo hayo yameifanya Nigeria na Bukina Faso kulingana kwa alama wote wakiwa na alama tano lakini wakizidiana kwa tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa.
Bukinabe sasa wanamsububiri mshindi wa pili wa kundi D ambaye atapatikana hii leo kati ya Togo au Tunisia.
Katika mchezo huo Collins Mbesuma aliungana na mshambuliaji wa Southampton Emmanuel Mayuka katika sehemu ya ushambuliaji ya Zambia, ambapo mshambuliaji huyo wa Orlando Pirates Mbesuma alikuwa akicheza nafasi ya nahodha Christopher Katongo ambaye unahodha wake ulikaimiwa kwa muda na mlinda mlango Kennedy Mweene.
Kocha Herve Renard alifanya badiliko moja la mchezaji pale alipomuingiza Hichani Himonde aliyechukua nafasi ya mlinzi mkongwe Joseph Musonda.
Kwa upande wa Bukinabe nahodha Moumouni Dagano aliendelea kusugua benchi kwa mara ya pili na nafasi yake kuchukuliwana Benjamin Balima.
Mlinda mlango Daouda Diakite alikuwa katika milingoti mitatu ya goli la Bukina Faso huku mlinda mlango namba moja Abdoulaye Soulama akiaangalia mpira kama mtazamaji kufuatia kusimama kwa mchezo mmoja baada ya kusimamishwa kwa kadi nyekundu na Florent Rouamba kuingizwa uwanjani kuchukua nafasi ya Aristide Bance.
Wakicheza katika vazi la rangi ya manjano na michirizi ya kijani Zambia walipata nafasi nzuri ya kuandika bao kunako dakika ya 17 pale ambapo kosa ya mlinzi wa Bukina Faso Mady Panandetiguiri lilipelekea mpira kunaswa na Mbesuma, lakini shuti lake lilikwenda moja kwa moja katika mikono ya mlinda mlango wa Mali, Diakite.

NIGERIA YAFUZU BAADA YA KUICHAPA ETHIOPIA.
Penati mbuli za dakika za mwisho mwisho zilizo pigwa na Victor Moses kunako dakika za 79 na 90 zimeisaidia Nigeria kukata tiketi ya kucheza robo fainali ya michuano ya mataifa ya Afrika baada ya kuibuka na ushindia mabao 2-0 dhidi ya Ethiopia.
Endapo Nigeria ingekwenda sare ya bila kufungana katika mchezo huo ilikuwa dhahiri shahiri wako nje ya michuano hiyo kutokana na sheria ya mfumo wa mchezo wa kiungwana (fair play system), ambapo bingwa mtetezi Zambia angefaidika na sheria hiyo.
Baada ya kuona dakika zikiyoyoma huku matumaini ya kupata bado yakitoweka, mashabiki wa Nigeria walianza kukata tama kufuatia timu yao kupata kazi ya kusawazisha katika dakika la mwisho michezo miwili iliyotangulia.
Hatimaye bahati ikawadondokea Nigeria kunako dakika ya 79 kufuatia kuangushwa chini katika eneo la hatari mshambuliaji Victor Moses na mlinzi Alula Girma kabla ya Moses mwenye kupiga penati hiyo na kuandika bao la kwanza.
Moses aliwahakikishia Nigeria alama tatu muhimu baada ya mlinda mlango wa Ethiopia Sisay kufanya madhambi ya kumkwatua mshambuliaji wa Nigeria katika eneo la hatari ambapo alitolewa nje kwa kadi ya pili ya njano ambao ilizaa kadi nyekundu na nafasi yake kuchukuliwa na Hintsa lakini Moses akafanikiwa kuandika bao la pili na kuifanya Nigeria kufuzu.