
Neno kubwa usiku wa jana lilikuwa ni REMONTADA ambalo lina maana ya kurejea. Na hiyo ilikuwa ni madre of all remontadas kwa tafsiri isiyo rasmi sana ni mama aliyerejea.
Endapo kama kulikuwa na wasiwasi wowote juu ya uwezo wa timu ya Barcelona msimu huu katika michuano ya vilabu bingwa Ulaya sasa imethibtika kuwa Barcelona ni alama nyingine kabisa yenye uwezo wa kipekee barani Ulaya.
Wote klabu yenyewe na wachezaji ni 'ma-genius' na wanamvuto wa kuangaliwa.
Lionel
Messi ndani ya kikosi cha Barcelona ni mchezaji bora kuliko wote katika duniani waliowahi kutokea na hakuna ubishi licha ya kwamba walikuwepo magwiji katika siku nyuma kama Diego Maradona, Johan Cruyff na Zinedine Zidane.
Ukienda mbali zaidi ni mchezaji mwenye bahati akitokea katika kikosi kitukufu na fahari kukichezea.
Mbao mawili aliyofunga usiku wa jana yalikuwa ni mabao yake ya 52na 53 msimu huu.
Si kweli kusema kwamba kila mchezaji mwenye kipaji anaweza kufunga akiwa amezungukwa na vipaji vingi lukuki vilivyo sheheni katika kikosi. HUYU NDIO MESSI.


Gerard Pique akipiga kelele za furaha baada ya Barca kuandika bao la pili lililofingwa na mtukufu Messi na goal aggregate kusomeka 2-2.
Messi is a phenomenon, daraja tofauti ambaye amekuwa akitoa tafsiri ya mechi kuliko mtu yoyote aliyeko katika kizazi cha sasa katika soka zaidi ya hata yule anayefananishwa naye Cristiano Ronaldo.
Barcelona ililazimika kushinda zaidi ya mabao mawili ili iweze kusonga mbele na ni Messi aliyefanya mazingira kuwa katika mstari ndani ya kipindi cha kwanza za mchezo na ndio maana anatajwa kama mtu anaye define mchezo.
Aliandika bao la kwanza kunako dakika ya 5 kabla ya kuongeza lingine kunako dakika ya 40 ambapo pia uhodari wa kumiliki mchezo wa Barcelona ukawa ndio dawa ya mafaniko.
Akicheza gonga za 'one-two' na mtaalamu mwingine wa dimba Xavi Hernandez ndani ya eneo la hatari la yard sita akizungukwa na wachezaji wa Milan haikuwa shida kwake kupiga mpira kwa guu lake la kushoto lililotinga wavuni na kumuacha mlinda mlango Christian Abbiati asijue la kufanya.
Bao la pili lilitokana na nahodha wa Milan
Massimo Ambrosini kuupoteza mpira na kunaswa na Andres Iniesta, ambaye alimpenyezea Messi ambaye aligeuka kushoto haraka na kupiga shuti la guu lake la kushoto na kupita katikati ya miguu ya mlinzi wa Milan Philippe Mexes na hatimaye kutinga wavuni huku Abbiati mara nyingine tena akigaa gaa bila matumaini.

Hivi ndivyo alivyo funga bao la pili.
WALIOTINGA ROBO FAINALI NI HAWA HAPA.
Bao la tatu lilitokana na mpira ulioanzia kwa Javier Mascherano aliyekuwa katikati ya uwanja na kuupeleka mpira kwa Iniesta, ambaye aliusogeza kwa Xavi na hatimaye David Villa aliyemalizia.
Bao la tatu lilitokana na mpira wa free-kick uliokuwa umbali wa yard 40 kutoka goli la Barcelona uliokuwa ukichezwa na wachezaji wa Milan Robinho na Sulley Muntari kupotea na kumkuta Messi na kuucheza mpira mrefu kwa Alexis Sanchez ambaye aliupiga kwenda kwa mlinzi wa kushoto Jordi Alba.
Barcelona
Borussia Dortmund
Galatasaray
Juventus
Paris St Germain
Real Madrid
Bayern Munich or Arsenal
Malaga or Porto
Borussia Dortmund
Galatasaray
Juventus
Paris St Germain
Real Madrid
Bayern Munich or Arsenal
Malaga or Porto
Bao la tatu lilitokana na mpira wa free-kick uliokuwa umbali wa yard 40 kutoka goli la Barcelona uliokuwa ukichezwa na wachezaji wa Milan Robinho na Sulley Muntari kupotea na kumkuta Messi na kuucheza mpira mrefu kwa Alexis Sanchez ambaye aliupiga kwenda kwa mlinzi wa kushoto Jordi Alba.


Messi akizungukwa na wachezaji wa Milan kaunga.

Tangu michuano ya European Cup kubadilika jina na kuwa Champions League, hakuna timu iliyofuzu ikiwa nyuma ya matokeo ya mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza na hatimaye kushinda na kupita katika mchezo wa marudiano na kisha kusonga mbele katika hatua ya mtoano.
Barcelona ndio pekee iliyofanikiwa kufanya hivyo mwaka 1994 ikiwa nyuma ya mabao 3-1 dhidi ya Dynamo Kiev in 1994.
Kushindwa kupata bao la ugenini kwa Milan kumigharimu Milan.







Jordi Roura akikaimu nafasi ya Tito Vilanova katika benchi la Barcelona.



Spotted: Ronnie Wood (of Rolling Stones fame) was seen in the crowd with wife Sally

We're a team! Barcelona fans' message of unity for their players ahead of the clash
No comments:
Post a Comment