Kikosi cha Ashanti kilichorejea ligi kuu. |
Ligi
Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa 2012/2013 unamalizika wikiendi hii huku
timu za Mbeya City ya Mbeya, Ashanti United ya Dar es Salaam na Rhino
Rangers ya Tabora zikiwa tayari zimepata tiketi ya kucheza Ligi Kuu ya
Vodacom (VPL) msimu ujao.
Leo jioni (Machi 16 ) katika kundi B kutakuwa na mchezo baina ya Green Warriors vs Polisi
Dar (Karume, Dar es Salaam) na Ndanda vs Villa Squad (Nangwanda Sijaona,
Mtwara).
Katika kundi C hii leo (Machi 16 ) Polisi Tabora vs Pamba (Ali Hassan
Mwinyi, Tabora).
Kundi
A mechi zote zitachezwa Jumapili (Machi 17 mwaka huu) ambapo Majimaji
vs Mbeya City kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea, Kurugenzi vs
Mkamba Rangers (Mafinga) na Burkina Faso vs JKT Mlale (Jamhuri,
Morogoro).
Keshokutwa (Machi 17 mwaka huu) ni Moro United vs Ashanti
United (Karume, Dar es Salaam) na Tranist Camp vs Tessema (Mabatini,
Mlandizi).
Keshokutwa (Machi 17 mwaka huu) ni Polisi Mara vs JKT
Kanembwa (Karume, Musoma), Polisi Dodoma vs Mwadui (Jamhuri, Dodoma) na
Rhino Rangers vs Morani (Ali Hassan Mwinyi, Tabora).
No comments:
Post a Comment