KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, June 20, 2013

LIONEL MESSI KIZIMBANI MWEZI SEPTEMBA NCHINI HISPANIA.



Mshambuliaji wa Barcelona raia wa Ajentina Lionel Messi atatakiwa kupanda kizimbani mwezi Septemba kusikiliza kesi dhidi yake ya ukwepaji wa kodi nchini Hispania.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 25 ambaye ametajwa mara nne kuwa mchezaji bora wa dunia pamoja na baba yake Jorge wanakabiliwa na mashitaka ya kukwepa kodi katika mamlaka za kodi nchini Hispania ya zaidi ya euro milioni 4 sawa na pauni milioni £3.4m sawa na shilingi bilioni 8.6 za kitanzania.

Inaarifiwa kuwa Messi aliyatumia makampuni ya huko Belize na Uruguay kuuza haki ya matumizi ya sura ya Messi.

Mshahara kamili wa Messi anaolipwa na Barcelona ni euro milioni 16 kwa mwaka na kumfanya kuwa mchezaji mwenye thamani kubwa zaidi duniani.

Messi ana mikataba mbalimbali na wadhamini wengi duniani.
Mchezaji huyo ana mikataba ya kutumia picha yake na makapuni ya Banco Sabadell, Danone, Adidas, Pepsi-Cola, Proctor and Gamble and the Kuwait Food Company.

Na endapo atapatikana na hatia basi huenda akaenda jela miaka sita na faini kubwa hii ikiwa ni kwa mujibu wa shirika la habari la Hispania Efe news agency.

No comments:

Post a Comment