KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, October 8, 2014

UKURUSA WA HABARI KIMATAIFA:Garreth Bale hataki Ronaldo kuondoka Madrid, Luis Suarez apongeza kitendo cha Cavani kutaka kuondoka PSG, Nafuu nyingine kwa Luis Van Gaal kufuatia kurejea dimbani kwa Michael Carrick ...................



Gareth Bale amesema hataki kuona nyota mwenzake Cristiano Ronaldo akiondoka Real Madrid kurudi Uingereza kwenye ligi ya Premier.
Licha ya Ronaldo kuendelea kufunga mabao ikiwemo matatu wikendi jana dhidi ya Athletic Bilbao yaliomfanya afikishe rekodi ya ‘hat-trick’ ya 22 katika La Liga  na kufikia rekodi  ya ligi iliyowekwa na wachezaji wa zamani Telmo Zarra na Alfredo Di Stefan.

Ronaldo amekuwa katika uvumi wa kutaka kurudi katika timu yake ya zamani ya  Manchester United msimu ujao wa kiangazi.
Hivi majuzi, zilizuka tetesi kuwa Ronaldo anaweza kurudi katika timu yake ya zamani ya United ua Manchester City na Bale ametangaza hataki nyota mwenzake arudi kwenye ligi ya Premier.
Amedhihirisha ni mchezaji wa kiwango cha kimataifa amekuwa anafunga mabao mengi.
Bila shaka, hatutaki aondoke na ninataka asalie hapa Real Madrid,” Bale alisema.
 &&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&
  
Luis Suarez apongeza kitendo cha Cavani kutaka kuondoka PSG

Mshambuliaji wa timu ya Barcelona Luis Suare ameunga mkono kitendo cha mshambuliaji mwenzake wa timu ya taifa ya Uruguay Edinson Cavani kutaka kuondoka katika timu ya PSG.
Suarez amemueleza Cavani anajishusha mwenyewe kwa kukubali kuwa nyuma ya Zlatan Ibranimovic katika timu  ya PSG.
Cavani amekuwa akihusishwa kutaka kwenda kujiunga na timu za Arsenal, Manchester United, Liverpool wiki hii aliyekuwa mshambuliji wa  Liverpool Suarez amesema  si kitu kizuri kuona wanamchezesha Cavan katika nafasi tofauti na nafasi yake.
Paris imefanya maisha kuwa magumu kwa Cavani ni bora aondoke.
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&

NTOTA WA MISRI AJIONDOA TIMU YA TAIFA TATIZO JERAHA

Mchezaji wa timu ya Hull City  ya nchini Uingereza Ahmed Elmohamady amejiondoa katika kikosi cha  cha timu ya taifa ya Misri kitakachokabiliana na timu ya Botswana katika mechi mbili za kufuzu katika fainali ya kombe la mataifa ya Afrika mwezi huu.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 alijeruhiwa wakati timu hiyo ilipopata ushindi katika mechi dhidi ya Crystal Palace siku ya jumamosi.
Timu ya Hull imesema kuwa mchezaji huyo anauguza jeraha la mgongo.
Misri itachuana na Botswana ugenini siku ya ijumaa na baadaye katika uwanja wa nyumbani siku tano baadaye huku shinikizo zikizidi dhidi ya Kocha Shawky Gharib baada ya timu hiyo kushindwa mara mbili katika kundi la G.
Timu hiyo ya Pharaoh haina pointi hata moja ,pamoja na timu ya Botswana na sasa inakabiliwa na kibarua kigumu kufuzu katika mechi za AFCON mwakani nchini Morrocco.
Siku ya jumanne Rais wa shirikisho la soka nchini Misri Gamal Allam alisema kuwa kushindwa kwa timu hiyo ya taifa ni jukumu la kamati yake ya kiufundi.
''Tutamuajiri meneja kutoka nchi za kigeni iwapo Gharib atashindwa kuipeleka timu hiyo katika fainali za mataifa ya afrika nchini Morocco mwakani alisema Gamal.
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&

BECKERNBAUER ANAENDELEA KUSHANGAA KILICHOPELEKEA QATAR KUPEWA UWENYEJI WA KOMBE LA DUNIA

Franz Beckenbauer amesema alishangazwa na hatua ya Qatar kushinda maandalizi ya kombe la dunia mwaka 2022.
Mchezaji huyo wa zamani wa kikosi cha Ujerumani ni miongoni mwa watu 22 walioamua ni wapi kinyang'anyiro hicho cha mwaka 2018 na 2022 kitafanyika katika kura iliofanyika mnamo mwezi Disemba mwaka 2010.
Akizungumza katika mkutano wa kuimarisha mchezo huo, mwaka 2014 ,Beckenbauer alikataa kusema ni nani aliyempigia kura ,ijapokuwa ilidaiwa kuwa alipendelea  fainali hizo zifanyike nchini Australia.
''Ilikuwa ni kura ya siri,nilishangaa kuona Qatar ikiibuka mshindi'',Alisema mchezaji huyo mkongwe.
Mchezaji huyo wa zamani ambaye alishinda kombe la dunia kama mchezaji na meneja wa timu ya Ujerumani ,aliongezea kuwa,ushindani ulikuwa mzuri,kama ile mingine lakini hakukuwa na tofauti kubwa.
Lazima kuna sababu kwa nini zile nchi nyengine hazikufanikiwa kuandaa fainali.
Beckernbeur enzi za uchezaji wake
Qatar iliishinda Australia,Japan ,korea kusini na Marekani katika kura ya kuandaa fainali za kombe la dunia  mwaka 2022,huku Urusi ikiishinda Uingereza pamoja na Ubelgiji na Uholanzi,Ureno na Uhispania kwa haki ya kuandaa kombe la dunia la mwaka 2018.
Ni kamati kuu ya FIFA ndiyo iliyotoa uamuzi huo ambao umekumbwa na utata tangu tangazo hilo lifanywe.
Wanachama wawili wa zamani wa Shirikisho hilo walizuiliwa kushiriki katika kura hiyo kutokana na madai ya ufisadi,huku wengine sita wakilazimishwa kujiuzulu baada ya kura hiyo.
Backenbauer alijiondoa katika kamati hiyo mnamo mwaka 2011.
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&


NJE YA SOKA NDANI YA CRICKET:
Charlotte Edwards kutoka Uingereza kushiriki katika tuzo za mwaka 2014.
Charlotte Edwards kutoka Uingereza kushiriki katika tuzo za mwaka 2014.
Baraza la kimataifa la mchezo wa Cricket limemtaja nahodha wa timu ya taifa ya wanawake ya mchezo wa Cricket  Charlotte Edwards kutoka Uingereza kushiriki katika tuzo za mwaka 2014.
Edwards, 34, ni mwanamke  pekee aliyetajwa katika orodha ya wachezaji wanaowania tuzo hiyo wengine ni nahodha wa Sri Lanka Angelo Mathews.
Mitchell Johnson kutoka Australia, Dale Steyn kutoka Afrika kusini na  Huvneshwar Kumar kutoka india.Tuzo hizo zitapigiwa kura na mashabiki wa mchezo huo kwa njia ya mitandao.
Mshindi wa tuzo hiyo atatangazwa jumatano ya November 5 Washindi wa tuzo zilizopita nyota wa India Sachin Tendulkar na Mahendra Dhoni, na kutoka Sri Lanka  Kumar Sangakkara.
&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&&


Nafuu nyingine kwa Luis Van Gaal kufuatia kurejea dimbani kwa Michael Carrick
Nafuu ya Luis van Gaal baada ya Carrick kuthibitika kurudi
Kocha wa Man United Louis Van gaal amesema kiungo wake MICHAEL CARRICK anajiandaa kurudi dimbani.
Kiungo huyo wa miaka 33 alikuwa nje ya uwanja kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya kifundo cha mguu.
Michael Carrick kurejea uwanjani
Kukosekana kwake kumesabisha kuyumba kwa kikosi cha kocha huyo hasa sehemu kiungo cha kati.
Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari  kocha Louis amesema kukosekana kwa kiungo huyo mkabaji kulisababisha kutofanya vizuri na hasa ikizingatiwa ana uzoefu katika soka.

No comments:

Post a Comment