KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, October 22, 2013

Akina Kalaba, Sunzu & Sinkala warejeshewa pasi zao za safari.

Serikali ya Zambian imewarejeshea pasi za kusafiria wachezaji watatu wa TPN Mazembe Rainford Kalaba, Stoppila Sunzu na Nathan Sinkala, na hivyo kumaliza mzozo ulioibuka kufuatia kushindwa kuungana na wenzao katika michezo miwili ya kimataifa.

Zambia iliwanyang'anya wachezaji hao pasi zao za kusafiria baada ya kushindwa kuelekea Beijing kwa ajili ya mchezo wa kimataifa dhidi ya Brazil nchini China wiki iliyopita ambapo sasa maafisa wa uhamiaji wamewarejeshea pasi zao na kwasiri vijana hao wamerejea katika klabu yao ya TP Mazembe ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Hta hivyo hii leo, Kalaba na Sunzu wamechukua makabrasha yao ilhali Sinkala akitakiwa kuchukua kutoka katika ofisi za uhamiahi za mjini Ndola.

No comments:

Post a Comment