Katika ligi ya Ujerumani Bundesliga , jana Jumapili(10.11.2013) kulikuwa
na michezo miwili ya kukamilisha duru ya 12 ya mchezo wa Bundesliga,
ambapo Stuttgart iliikaribisha Freiburg. VFB Stuttgatr iliikabidhi
Freiburg kipigo cha mabao 3-1 na kupanda hadi katikati ya msimamo wa
ligi hiyo.
Mainz 05 ikapata ushindi wa jasho wa bao 1-0 dhidi ya
Eintracht Frankfurt ikiwa ni ushindi wa dakika za mwisho.
Choupo-Moting alipachika bao hilo la ushindi zikiwa zimesalia sekunde
120 mchezo kumalizika.
Hata hivyo mlinda mlango chipukizi wa Mainz 05
Loris Karius ambaye alikuwa langoni badala ya kipa namba moja Heinz
Müller ambaye ni majeruhi na kipa namba mbili Christian Wetklo ambaye
ana kadi nyekundu alifanya kazi nzuri kulinda ushindi huo.
"Sikuwa na wasi wasi. Nilikuwa nafahamu kwa siku kadha kuwa nitacheza
na nimejaribu, kuweka yote hayo pamoja. Nilikuwa na hisia kuwa itakuwa
siku nzuri.Kwa hiyo nilifanya kila linalowezekana."
Siku ya Jumamosi FC Bayern iliiadhibu FC Augsburg kwa mabao 3-0 na
kuendelea kujikita kileleni mwa Bundesliga baada ya makamu bingwa wa
ligi hiyo Borussia Dortmund kuteleza , baada ya kuzabwa mabao 2-1 na
Wolfburg. FC Bayern imeendelea kuvunja rekodi moja baada ya nyingine
msimu huu, ambapo wiki hii iliivuka rekodi ya kale iliyokuwa imewekwa na
Hamburg SV na kupata ushindi katika michezo 37 ya ligi bila kushindwa.
Leverkusen imeendelea kubakia katika nafasi ya tatu baada ya kupata
ushindi mnono wa mabao 5-3 dhidi ya Hamburg SV. Mshambulia Son
alipachika mabao 3 dhidi ya timu yake hiyo ya zamani.
Schalke 04 nayo ilijipatia ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Werder Bremen.
No comments:
Post a Comment