Katibu mkuu wa shirikisho la kandanda duniani FIFA Jerome Valcke
anakutana na waziri wa michezo wa Ghana pamoja na maafisa wengine
nchini Togo leo kuwahakikishia mipango wa usalama kwa ajili ya mchezo wa
mtoano katika kinyang'anyiro cha kuwania tikiti ya kucheza katika
fainali za kombe la dunia mwakani nchini Brazil mchezo ambao utafanyika
mjini Cairo wiki ijayo.
Ghana ilisema kuwa inahofia usalama nchini Misri baada ya mara kwa mara
nchi hiyo kukumbwa na maandamano na huenda mashabiki wa Misri wakafanya
maandamano dhidi ya utawala wa kijeshi nchini humo katika uwanja wa
mjini Cairo wa Juni 30 ambao unamilikiwa na jeshi.
No comments:
Post a Comment