Barcelona ya Uhispania imempoteza Lionel Messi , ambapo ni majeruhi kwa
mara nyingine tena lakini pamoja na hayo waliweza kushinda pambano lao
dhidi ya Real Betis kwa mabao 4-1 na timu inayoifukuzia kwa karibu
Atletico Madrid iliteleza baada ya kutoka sare ya bao 1-1 jana Jumapili
dhidi ya Villareal.
Messi alipata maumivu ya misuli ya paja na atakuwa nje ya uwanja kwa wiki 6-8 .
Hakuna shaka amesema kocha wa mabingwa hao wa la Liga Barcelona Gerardo
Martino kuwa watazungumza na Messi na kuhakikisha kuwa maumivu hayo
hayatamfanya kuingiwa na hofu na kumuathiri kiakili.
No comments:
Post a Comment