KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, January 9, 2013

KELVIN YONDANI NA FRANK DOMAYO KUUNGANA NA KIKOSI CHA KILI TAIFA STARS ADDIS ABABA MOJA KWA MOJA. STARS KUODOKA MCHANA WA LEO KUWAFUATA ETHIOPIA.

Wachezaji wa Kili taifa Stars mara baada ya mazoezi asubuhi ya leo.
Wachezaji wa wawili wa Yanga Kelvin Yondan na Frank Domayo sasa watalazimika kuelekea moja kwa moja nchini Ethiopia wakitokea nchini Uturuki kuungana na wachezaji wengine wa timu ya taifa ‘Kili taifa stars’ ambayo inaondoka nchini mchana wa leo kuelekea nchini humo kwa mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya nchi hiyo mchezo ambao umepangwa kufanyika keshokutwa tarehe 11/01/2013.

Hayo yameelezwa na meneja wa timu ya taifa Leopard Tasso Mukubezi alipokuwa akiongea na Rockersports asubuhi hii wakati stars walipokuwa wakifanya mazoezi ya mwisho mwisho kabala ya safari mchana wa leo.

Taso amesema Kelvin Yondani na Frank Domayo wameshindwa kupata usafiri wa kuwaleta nchini na kuwahi safari na wenzao hivyo wamelazimika kubadilisha safari ya nchini Tanzania na sasa watakuwa safarini wakielekea nchini Ethiopia.

Kocha wa Kili taifa stars Kim Poulsen kupitia shirikisho la soka nchini TFF aliwaomba wachezaji wawili kati ya watano wa Yanga ambao wako katika kikosi cha Yanga kinachoendelea na kambi Antalya nchini Uturuki ili kuongeza nguvu katika kikosi cha timu ya taifa kitakacho cheza na Ethiopia.

Wachezaji wengine wa stars kutoka Yanga ambao wamesalia Antalya ni Nadir Haroub Kanavaro, Athumani Iddi Chuji na Simon Msuva ambao taarifa zinasema wataungana na kambi ya Kili taifa stars mara baada ya Yanga kumaliza ziara yao ya kambi nchini Uturuki.

Wachezaji watatu wa Azam Salum Abubakar, Mcha Khamis na Aishi Manula wao walijiunga na kambi ya timu ya taifa tangu jana na leo wameshiriki mazoezi ya asubuhi kabla ya safari ya Ethiopia mchana wa leo.

Mpaka sasa kambi hiyo ina jumla ya wachezaji 16 wakiwepo wachezaji wengine kutoka Simba Juma Kaseja, Mrisho Ngasa, Amri Kiemba, Amir Maftaha, Mwinyi Kazimoto na Shomari Kapombe.

Wengine ni Aggrey Moris na Erasto Nyoni wa Azam fc ambao walijiunga na kambi hiyo tangu mapema kwakuwa wapo jijini Dar es Salaam kutokana kusimamishwa na klabu yao ya Azam kwasababu za kuhusishwa na tuhuma upangaji wa matokeo.

 Wachezaji wengine ni Shabani Nditi , Issa Rashid wa Mtibwa,  Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe timu ya Taifa itaondoka kesho saa tisa kwa mchezo mmoja dhidi ya Ethiopia tarehe 11/01/2013 ukiwa ni mchezo wa maandalizi ya mchezo wake wa kuwania fainali ya kufuzu kombe la dunia mwezi machi dhidi ya Morocco.

Wao Ethiopia wanajiandaa kwa ajili ya fainali za mataifa ya Afrika nchini Afrika kusini na wanatarajia kuanza mchezo wao wa kwanza dhidi ya mabingwa wa soka barani Afrika Zambia tarehe 21 mchezo wa kundi C katika uwanja Mbombela.

No comments:

Post a Comment