KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, March 17, 2014

Mutai ampiku Mo Farah New York

Bingwa Mtetezi wa mbio za New York Marathon Geoffrey Mutai alitoka nyuma na kuthibitisha udedea wake katika barabara za mji huo wa Marekani alipokata utepe akitumia muda wa saa moja na sekunde hamsini.
Muingereza Mo Farah, hata hivyo, ndiye aliyewaduwaza mashabiki wake nchini Marekani alipokunguwaa na kuanguka baada ya takriban kilomita tisa na kisha akajifua na kurejea kwa kishindombio zikikaribia kukamilika .
Bingwa huyo wa mbio za mita elfu tano na mita elfu kumi za olimpiki alimaliza katika nafasi ya pili sekunde 18 pekee nyuma ya Mkenya mshikilizi wa muda bora katika mbio za marathon duniani.
Farah alishikwa na kisunzi punde baada ya kukamilisha mbio hizo na alilazimika kubebwa kwa machela.
Mo Farah azirahi baada ya kukamilisha mbio za New York

Muingereza huyo baadaye alisema alikuwa sawa na kuwa ataendelea na mazoezi yake kabla ya kushiriki mbio zake za kwanza za marathon katika mashindano ya London Marathon zitakazoandaliwa mwezi ujao.
Mkenya mwengine Stephen Sambu alimaliza katika nafasi ya tatu sekunde moja pekee nyuma ya Mo .
Ilikuwa siku njema kwa wakenya kwani Sally Kipyego vilevile kutoka Kenya alitwaa ubingwa wa kitengo cha wanawake akisajili muda wa saa moja dakika 8 na sekunde 31.
Muda huo ndio wa kasi zaidi katika kitengo hicho cha wanawake.
Bizunesh Deba, kutoka Ethiopia alimaliza wapili huku Mmarekani Molly Huddle akikamilisha orodha ya tatu bora.
Wanariadha 20,000 walistahimili kiwango cha nyuzijoto zaidi ya 30 na kushiriki mbio hizo za kilometer 21 .

No comments:

Post a Comment