KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, July 29, 2014

Zama zimeanza kurudi:Kesho uwanja wa Mkwakwani ni vita, watani wa jadi wa mkoa wa Tanga, hapa Kimanumanu kule wagosi wa kaya...

Mashabiki wa soka wa mkoa wa Tanga kesho watakuwa na burudani ya aina yake pale vilabu vya vikubwa Coastal Union na African Sports vitakapo uumana kutoa burudani ya Idi
TIMU za Coastal Union (Wagosi wa Kaya) na African Sports (Wanakimanumanu) zote kutoka mkoani Tanga kesho kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani watatoa burudani ya kumalizika mwezi mtukufu wa Ramadhani ikiwa ni siku ya idi pili.

 

Taarifa ya msemaji wa Coastal Union kwa mtandao wa Rockersports, Oscar Assenga imesema maandalizi ya kuelekea  mchezo huo yamekamilika kwa asilimia kubwa na kinachosubiriwa na mechi hiyo itakayoanza saa kumi jioni kwenye uwanja huo.

Akiongea na mtandao huu kocha wa Coastal Union Yusufu Chipo amesema baada ya kumaliza mechi hiyo timu hiyo itaelekeza mipango yake ya kucheza mechi za kirafiki nyengine ili kuweza kujiweka imara kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara.

Amesema wachezaji wa timu hiyo wataingia kwenye mechi hiyo kwa malengo ya kupata ushindi ili kuweza kuendeleza rekodi ya kuwafunga wanakumanumanu hao ambao msimu ujao watashiriki michuano ya ligi daraja la kwanza.

Kwa upande wake afisa Habari wa African Sports Said Karsandas amesema kuwa wamepania kushinda kwenye mechi hiyo ili kuweza kurudisha ile heshima ya timu hiyo kwa wagosi hao wa kaya.

Kumbuka African Sports ambayo iliwahi kuwa tishio katika soka la Tanzania miaka ya mwishoni ya 1980' hivi sasa inapambana kurejea ligi kuu ya Soka Tanzania bara na inajiandaa na ligi daraja la kwanza ambayo inatarajia kuanza mapema mwezi wa Septemba.

No comments:

Post a Comment