KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, September 25, 2014

Asamoah Gyan akana madai ya kafara

Nahodha wa timu ya taifa ya Ghana, Asamoah Gyan, amekanusha madai kuwa alimtoa kafara yake ambaye pia alikuwa mwanamuziki mashuhuri nchini Ghana Castro.
Gyan amesema tetesi hizo ni za kushangaza sana wala hazina msingi.
Mwanamuziki huyo aliyekuwa anaiimba nyimbo za mtindo wa Afrobeats, ambaye jina lake halisi ni Theophilus Tagoe, alitoweka pamoja na rafiki yake Janet Bandu, mnamo mwezi Julai.
Wawili hao walitoweka wakati walipokuwa wamekwenda likizo na Gyan ambaye alikuwa mchezaji wa zamani wa Sunderland, katika mji wa Ada.
Madai katika vyombo vya habari nchini Ghana yanasema kuwa kutoweka kwa rafiki ya Gyan kumezua wasiwasi baadhi wakidai kuwa huenda alimtoa kafara mwanamuziki huyo.
Castro na rafiki yake Bandu, walionekana kwa mara ya mwisho wakielekea baharini na baadaye iliarifiwa kuwa walizama.
Miili ya wawili hao haikuwahi kupatikana na madai yaliendelea kusambazwa mwezi huu wakati ambapo kakake Gyan, Baffour Gyan alidaiwa kuwa mmoja wa genge la vijana waliowashambulia wandishi wa habari waliohoji maswali kuhusu madai hayo.
Hata hivyo baadaye aliachiliwa na polisi waliokuwa wamemkata kwa lengo la kumfungulia mashitaka.
Tetesi hizo zilimfanya Gyan kuitisha mkutano na wandishi wa habari kuzungumzia madai hayo.
Wakili wake Kissi Agbyabeng alitoa taarifa akisema kuwa familia ya Gyan imeshangazwa sana na madai hayo na iliamua kutosema chochote ili polisi waendelee na uchunguzi wao.
Taarifa hiyo ilisema: " Tumekuwa kimya huku madai na tetesi zikienezwa kila upande katika vyombo vya habari. Tumekuwa kimya sio eti kwa sababu tunaficha ukweli, bali kwa sababu hatuoni umuhimu wa kusema kilichojiri mjini Ada. Tumekuwa kimya kwa sababu tunataka polisi wafanye kazi yao bila kuingiliwa.''

No comments:

Post a Comment