KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, November 1, 2014

City Manuel Pellegrini ametanabaisha kwanini alimkosa Angel Di Maria

Meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini ametanabaisha kuwa mabingwa hao wa 'Premier League' hawakuweza kumsajili Angel Di Maria kutokana na sheria ya fedha FFP ( Financial Fair Play).
Muajentina huyo alijiunga na Manchester United kwa uhamisho wa rekodi ya kingereza ya pauni milioni £59.7 mwezi Agosti ambapo amekuwa akifanya kazi nzuri tangu wakati huo akifunga magoli matatu na kutoa pasi za mwisho za magoli.

Pellegrini ametanabaisha kuwa baada ya faini ya FFP klabu yake hawakuweza tena kulingania na ada iliyotolewa kwa ajili ya mshambuliaji huyo wa zamani wa Real Madrid.

"nadhani ni rahisi sana," amewaambia waandishi. "tulikuwa na zuio muhimu kuhusiana na bajeti yetu mwaka huu. Tusingeweza kutumia pesa ambayo United ilitoa kwa ajili ya Di Maria "

Di Maria atakuwepo uwanjani katika kikosi cha United watakapokuwa safarini Etihad mchezo wa 'Manchester derby' ya kwanza msimu huu, huku Wayne Rooney akijipanga kuungana naye katika kikosi cha kwanza baada ya kusimama kwa michezo mitatu.

No comments:

Post a Comment