KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, June 26, 2012

Chama cha soka Ujerumani cha pigwa faini.

Mashabiki wa timu ya taifa ya Ujerumani
Mashabiki wa soka nchini Ujerumani walioko katika michuano ya Euro wamekiponza chama chao cha soka kufuatia kupigwa faini ya Euro 25,000 na shirikisho la soka barani Ulaya UEFA kutokana na vurugu za mashabiki wake.
Mashabiki wa Ujerumani wametuhumiwa kwa kitendo cha kuonyesha mabango yaliyokuwa yakiuunga mkono neo-Nazi katika mchezo wa hatua ya makundi dhidi ya Denmark ikiwa na pamoja kuwasha moto na kuimba nyimbo za kibaguzi.

UEFA imeikabili DFB na kuwapiga faini hapo jana baada ya kubaini kuwa vitendo vya mashabiki hao ni kinyume cha maadili ya kisoka.
Taarifa ya UEFA inasomeka
 "chama cha soka cha Ujerumani (DFB) kimepigwa faini ya euro 25,000 na bodi ya kudhibiti vitendo vya kinidhamu ya UEFA ".

No comments:

Post a Comment