KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, June 26, 2012

FA yakemea mitusi kwa Cole na Young kupitia Twitter

 Chama cha kandanda nchini Uingereza FA kimeamua kuingilia kati mashambulizi ya ujumbe wa matusi kuelekea kwa wachezaji wawili Ashley Young na Ashley Cole kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter na kukemea huku kikisema hali hiyo haikubaliki.
Cole na Young wote walikosa penati katika mchezo wa jumapili wa robo fainali dhidi ya Italia na simba watatu kutolewa mashindanoni huku wachezaji hao wakianza  kutupiana matusi kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter
Taarifa ya FA imesema
"tunaingilia kati moja kwa moja taarifa zinazohusu kutuwa matusi wachezaji hawa wawili wa timu ya taifa ya Uingereza Ashley Cole na Ashley Young kupitia Twitter,''.
"wamejitolea kila kitu kwa timu yao ya taifa katika Euro 2012 inatisha na haikubaliki jumbe za aina hiyo ya matusi kutumwa.
Tunaunga mkono uchunguzi wa polisi ili kubaini nani anachochea hili.''
Msemaji wa polisi “Metropolitan Police Service” amenukuliwa akisema
 "tunafuatilia juu ya maoni ya kibaguzi kupitia Twitter katika mchezo wa usiku wa jana na tumeanza uchunguzi.
"uchunguzi ulianza kufanywa na MPS jana na mjumbe mmoja wa uchunguzi wa kufuatilia maoni kupitia mtandao wa kijamii wa twitter hususani maoni yanayotoka jijini London.
Hakuna mtu mpaka sasa aliyewekwa kizuizini kuhusiana na hilo. MPS inaangalia uwezekanao wa kufungua mashtaka kupitia kifungua 18/19 Public Order Act 1986.''
Watumiaji wa Twitter waliendelea kutoa maoni yao kuwakosoa  Young na Cole lakini baadae ikaandikwa
"ninachoweza kusema yote hayo ni utani jamani achaneni na hili, police wanajua nilikuwa natania na nina matumaini hawatanisumbua, cheers.''
Mwanafunzi mmjoa toka Wales  Liam Stacey aliwahi kwenda jela kwa siku 56 mapema mwaka huu kwa kumdhihaki kibaguzi wa rangi kiungo wa Bolton Fabrice Muamba baada ya kupoteza fahamu uwanjani katika mchezo dhidi ya Tottenham Hotspur.

No comments:

Post a Comment