Ibrahimovic: Paris Saint-Germain ni
bora kuliko AC Milan
Zlatan
Ibrahimovic ambaye ameanza kuitumikia timu yake mpya ya PSG anasema ameona
mengi katika timu yake hiyo kiasi kusema ni bora kuliko Milan.
Amenukiliwa
akisema Paris Saint-Germain ni bora kuliko timu yake ya zamani ya AC Milan.
Kufuatia mchezo
mmoja wa hapo jana wa kirafiki dhidi ya D.C United ambao ulimalizika kwa sare
ya bao 1-1 aliulizwa ni timu ipi bora kati ya timu yake ya sasa na ile ya
zamani Ibrahimovic alijibu kuwa timu yake ya sasa ndio bora
Mapemwa mwanzoni
mwa mwezi huu PSG ilifanya usajili muhimu (double swoop) kwa Ibrahimovic na
mlinzi wa Kibrazil Thiago Silva ambao uliwagharimu wamiliki raia wa Qatari
kiasi cha euro milioni 62.
Kwasasa Silva
yuko na kikosi cha Brazil kwenye michezo ya Olympic huku Ibrahimovic akiwa na
PSG na jana akicheza mchezo wake wa kwanza wa kirafiki dhidi ya D.C United
ambapo alifinga bao lake la kwanza akiwa na timu hiyo katika dakika ya tatu ya
mchezo.
Kama ilivyokuwa
kwa AC Milan timu ya zamani ya Ibrahimovic PSG pia alishindwa kupata taji
lolote katika msimu wa 2011-12 lakini
kwa kuwaongeza wachezaji wawili wa Milan pamoja na kiungo wa Pescara, Marco
Verratti pamoja na mshambuliaji wa Napoli Ezequiel Lavezzi, Ibra amejenga matumaini
makubwa kwa PSG.
Zote Milan na
PSG ziko katika hatua ya makundi ya michuano ya vilabu bingwa ulaya 2012-13.
Montolivo akanusha hoja juu ya
kuvurugika kwa AC Milan.
Riccardo
Montolivo amesisitiza kuwa AC Milan itaendelea kuwa moto licha ya kuhama kwa
wachezaji wake muhimu kama Zlatan Ibrahimovic na Thiago Silva msimu huu.
Milan
maarufu kama Rossoneri imeuza wachezaji wake muhimu kwenda Paris Saint-Germain mapema
mwezi huu wa July huku wakongwe kama Gennaro Gattuso, Clarence Seedorf, Filippo
Inzaghi, Gianluca Zambrotta na Alessandro Nesta wakiachwa katika jaribio la
kusuka upya kikosi cha timu hiyo.
Lakini pamoja
na klabu hiyo kuchukua uamuzi huo bado Montolivo ambaye ni miongoni mwa wachezaji wapya
ndani ya klabu hiyo anaamini kuwa San
Siro itaendelea kuwa juu katika msimu mpya.
Amenukuliwa na
Gazzetta dello Sport akisema
"si
dhani kama Milan iko kwenye shida kubwa kwa kufanya maamuzi hayo, ni kweli
klabu imepoteza wachezaji muhimu Milan ni klabu kubwa kabla ya Ibrahimovic na
Thiago na tutandelea kuwa hivyo hata bila ya wao."
Messi Apiga hat-trick na kuizamisha Raja
Casablanca 8-0
Lionel Messi
ameanza tena shughuli yake ya kupiga ‘hat-trick’ akiwa na kikosi chake cha Barcelona
baada ya kuchapa bao 8-0 Raja Casablanca ya Morroco katika mchezo wa kirafiki kule
Grand Stade mjini Tangier.
Alexis
Sanchez alianza kufunga bao la kwanza kabla ya Messi kupiga mawili. Wawili hao wakaendelea
kuinyanyasa Raja Casablanca huku Messi akiendelea kufanya kazi yake kuifanya Barcelona
kuongoza kwa mabao 4-0 na Messi akikamilisha hat-trick wakati wa
mapumziko.
Dani Alves
naye alifanikiwa kufunga na kuingia kwenye kitabu cha mabao akifunga bao la penati
kunako dakika ya 58 kabla ya nyota vijana Sergi Roberto na Gerard Deulofeu kuongeza
mengine mawili katika dakika tatu za mwisho za mchezo.
Baada ya
mchezo bosi mpya wa Barcelona Tito Vilanova amempongeza Messi katika mchezo wake
huo wa kwanza wa matayarisho ya kunza
kwa msimu mpya kufuatia kukosekana katika
mchezo wa kwanza dhidi ya Hamburg uliofanyika jumanne.
Amenukuliwa Vilanova
akisema
"unapokuwa
na mchezaji bora wa dunia mwenye uwezo mkubwa wa kufunga huo anaonyesha tofauti,
na kwa mara nyingine tena ameonyesha hilo,"
"mchezo huu ulikuwa mzuri kwasababu
tumecheza na timu ambayo inakimbiza na hata wachezaji vijana wamecheza vizuri
usiku huu."
Messi mwenyewe
akiongea na El Mundo Deportivo amesema
"kwa
muda mrefu sijapata kucheza mchezo wa matayarisho ya msimu kutokana na
kuchelewa kufika kwangu ilikuwa ni fursa nzuri kwani nimetoka katika mapumziko
ya muda mrefu.
Rodgers: Carroll anataka kusalia
Meneja wa Liverpool
Brendan Rodgers amesisitiza kuwa Andy Carroll
ni mwenye furaha na anataka kuendelea kusalia Liverpool na anataka kuzoea aina
mpya ya mchezo ambao unafundishwa katika klabu hiyo yenye maskani yake Anfield.
Kwasasa kumekuwepo
na tetesi kuwa Carroll huenda akaondoka Liverpool baada ya kuhangaikia kusaka
nafasi ya kucheza tangu kujiunga kwake na klabu hiyo akiatokea Newcastle United
kwa ada ya pauni milioni £35 mwezi januari 2011.
Klabu yake
ya zamani imekuwa katika harakati za kumrejesha carroll st james' park lakini
mpango huo ulikataliwa na wekundu hao wa london.
West Ham pia
imetenga pauni milioni £2 kumchukua Carroll kwa mkopo mpaka kumalizika kwa msimu
wa 2012-13 lakini pia kwa mpango wa kudumu wa pauni milioni £16 ikiwa klabu
hiyo itaepuka balaa la kushuka daraja.
Lakini Rodgers
bado anamtaka mshambuliaji huyo kuendelea kutoka mchango wake katika timu hiyo
na jana akiingia akitokea benchi katika mchezo wa kujiandaa na ligi dhidi ya Tottenham
uliomalizika kwa sare ya bila kufungana.
Jack Wilshere kuwa nje mpaka October
Kocha wa Arsernal
Arsene Wenger amesema Jack Wilshere hatakuwa
dimbani akitoa huduma katika klabu hiyo mpaka mwezi October.
Kiungo huyo
mwenye umri wa miaka 20 wa England alikosekana katika msimu mzima wa 2011-12 akisumbuliwa
na na ankle na alifanyiwa upasuaji mdogo mguu mwezi May mwaka huu.
Amenukuliwa Wenger
baada ya mchezo wa mwisho wa ziara yao ya barani Asia akiwa katika jiji la Hong
Kong akisema
"tunaimani ya kuwa tena Wilshere mwezi October,"
"na kwa
kuwa Abou Diaby amerejea , itakuwa ni kama tumesajili wachezaji wawili wapya. Kikosi
kitakuwa shupavu na kimashindano."
Wilshere alipatwa
na ankle kiangazi mwaka uliopita na amefanyiwa upasuaji wenye mafanikio na
mwenyewe ana matumaini kuwa katika nafasi ya kuanza mazoezi mepesi mwezi August
lakini katika hali nzuri mwezi October.





No comments:
Post a Comment