Baada ya shirikisho la soka Tanzania Tff kuingia mkataba wa miaka mitatu na
benki ya BancABC Juu ya kuanzishwa kwa
michuano mipya itakayoshirikisha jumla ya timu nane uongozi wa klabu ya simba
umelishangaa shirikisho hilo kwa kukurupuka
bila kushirikisha vilabu husika .
TFF ilitangaza kuwa kuanzia August 4 mpaka 18 timu bora tatu za bara na tatu
za Zanzibar pamoja na timu moja moja zilizopanda daraja msimu huu kucheza ligi
kuu kwa pande zote mbili Zanzibar na bara zitashiriki michuano hiyo iliyopewa
jina la BancABC SUP8R soccer Tournment 2012.
Makamu
mwenyekiti wa klabu ya Simba Geofrey Nyange ‘Kaburu’ akiongea na Rockersport.com amesema pamoja na
kupokea barua kutoka TFF juu ya kuwepo kwa mashindano hayo , klabu yake imeshaliandikia
barua shirikisho hilo wakiwapa masharti ili waweze kushiriki michuano hiyo huku akionyesha kutokuwa tayari kushiriki mashindano hayo .
Kaburu
amesema moja ya masharti hayo ni kutaka TFF ikutane na vilabu husika kabla ya kuanza kwa
mashindano hayo kwa kusema inashangaza TFF imeingia mkataba binafsi bila
walengwa kushirikishwa.
Akiendelea
zaidi kaburu amesema katika barua waliyopokea TFF inaeleza kuwa vilabu
vitaambulia asilimia 25 ya mgawo wa mapato huku TFF wakiondoka na asilimia 50.
Ameshangaa
kwa kuuliza kuwa inakuwaje michuano yenye udhamini TFF wajichotee asilimia
kubwa lakini pia akashangaa kulikoni wao kama watangazaji wa biashara ya
wadhamini wakapata mgawo mdogo,
Kama
haitoshi Kaburu amesema michuano hiyo
inaonekana haina tija kwa sababu ni mshindi wa kwanza pekee anayepata zawadi
huku zingine zikiwa hazina kitu.
Amesema
endapo TFF itashindwa kukutana na vilabu na kuzungumzia michuano hiyo na
masuala mazima ya maslahi kwa vilabu husika Simba kamwe haiwezi kushiriki.
Mbali ya
hivyo Kaburu amedokeza kuwa ukiangalia kwa undani michuano hiyo imeibuliwa tu
kwa sababu haipo kwenye kalenda ya TFF lakini kama haitoshi akaongeza kuwa Simba
tayari wameshashiriki michuano ya aina mbili kwa sasa walianza na michuano ya
ujirani mwema wakawa mabingwa na kisha
wameshiriki michuano ya Kagame ambapo wametolewa katika hatua ya robo fainali
na Azam ,
Kaburu
ameongeza kuwa kiufundi si vizuri kushiriki michuano ndani ya michuano hali inayopelekea timu
kutokuwa nzuri na kwenda tofauti na program ya kocha wao.
TFF
imezitaja timu za Simba, Yanga , na Azam pamoja na timu moja iliyopanda daraja
la kwanza kushiriki michuano kama ilivyo kwa upande wa Zanzibar.
Michuano
hiyo imepangwa kwa mtindo wa makundi mawili na itachezwa kwenye miji ya Dare s
salaam, Mwanza , Arusha na Zanzibar.

No comments:
Post a Comment