Ushindi wa
mabingwa watetezi wa michuano ya kombe la Kagame Dar es salaam Yanga Afrika dhidi ya Azam Fc hapo jana jumamosi umelezwa kuwa ulichangiwa kwa kiasi kikubwa na
Mweyekiti wa Klabu hiyo Yusuph Manji .
Akizungumza
na Rockersport Mmoja wa watu waliokuwa karibu na kambi ya yanga amesema , siku moja
kabla ya mchezo huo yaani ijumaa asubuhi Manji akifuatana na viongozi wenzake wa klabu waliwatembelea wachezaji
katika kambi yao kwenye Hotel ya Double Tree iliyopo Masaki nje kidogo ya
jijiji la Dar es salaa, awali wachezaji wa yanga walikuwa wakiishi kwenye hotel
ya Valley View iliyopokaribu kabisa na makao makuu ya klabu hiyo mitaa ya
jangwani.
Imeelezwa kuwa baada ya Manji na msafara wake kufika
hotelini hapo , waliweza kuzungumza na makocha pamoja na wachezaji na katika
mazungumzo hayo Manji aliwauliza wachezaji
bingwa wa michuano ya kombe la Kagame anapata nini ?
Wachezaji
walimjibu anapata dola elfu 30, kutokana na kauli ya wachezaji, Manji aliwaambia kuwa endapo watafanikiwa
kuutwaa ubingwa huo basi pesa zote ziwe mali yao naye akawaahidi kuwaongezea milioni kumi na tano
kama zawadi yake kwa wachezaji endapo watatwaa ubingwa.
Kama haitoshi
Manji pia akawaambia viongozi wenzake nao watoe ahadi zao kwa wachezaji
ambapo nao wakatoa ahadi mbali mbali za
fedha na kisha msafara huo ukaondoka .
Kutokana na
hali hiyo imeelezwa morari ya wachezaji na benchi zima la ufundi ikapanda zaidi
na kila mchezaji akaahidi kuwa endapo atapata nafasi ya kucheza fainali hiyo atapigana
kufa na kupona kuhakikisha Yanga inatwaa ubingwa na juhudi zao zikaisaidia Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 2 - 0
dhidi ya Azam hivyo Yanga kwa mwaka wa pili mfululizo kutangazwa kuwa mabingwa
wa michuano ya kombe la Kagame.
Kwasasa wachezaji wa Yanga wamekwenda mapumziko na watarejea kambini ijumaa kuendelea na mazoezi.


No comments:
Post a Comment