KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, July 13, 2012

KAMPENI YANGA VIPEPERUSHI VYATEMBEA MANJI MWENYEKITI CLEMENT SANGA MAKAMU WAKE .BIN KLEB,KATABALO,NYAMBAYA NA MANYAMA WAHUSISHWA

Fransis kaswahili
Ikiwa imesalia siku moja kabla ya uchaguzi mkuu mdogo wa kujaza nafasi za wajumbe wa kamati ya utendaji ya Yanga kufanyika, kamati ya uchaguzi ya Yanga imesema mwanachama yoyote atakaye elekea mahakamni kwa lengo la kujaribu kuzuuia uchaguzi huo kufanyika atafutwa uanachama wake ndani ya klabu hiyo na kuhukumiwa kwa mujibu wa kanuni za fifa .
kauli hiyo imetolewa na katibu wa kamati ya uchaguzi ya Francis Kaswahili wakati akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu hiyo kufuatia tishio la baadhi ya wanachama la kutaka kuelekea mahakamani kupinga kile kinacho daiwa ni kuenguliwa kwa baadhi ya wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya Yanga.
Hata hivyo Kaswahili ameshindwa kutaja majina ya wanachama hao huku tayari tetesi zikizagaa juu ya kuwepo kundi Fulani la wanachama waliojipanga kuelekea mahakamni kuzuia uchaguzi kufanyika tarehe 15/07/2012 kama ilivyotangazwa na kamati ya uchaguzi ya Yanga.
Lakini wakati hayo yakiwa hivyo kamati hiyo imepokea malalamiko ya kuwepo kwa kampeni chafu ambazo hata hivyo ameshindwa kuzithibitisha kuwa zimekuwa zikifanywa na nani mbali ya kuonyesha kipeperushi ambacho kimeonyesha majina ya baadhi ya wagombea na kikieleza kuwa hao ndio viongozi watakao iongoza Yanga.
Kaswahili amesema endapo watabainika wanao fanya kampeni ya aina hiyo adhabu itatolewa.
kipeperushi hicho kina majina ya wagombea na nafasi zao kama ifuatavyo
mwenyekiti –Yusufu Manji
makamu mwenyekiti- Clement Sanga
wajumbe – Katabalo
-        Nyambaya
-        Manyama
-        Bin Kleb
Aidha kuelekea kwenye uchaguzi jumapili kamati hiyo ya uchaguzi ya Yanga imesema ifikapo kesho kesho saa nane mchana ndio itakuwa mwisho wa kulipa ada kwa wanachama .
Siku ya uchaguzi milango itafunguliwa saa tano zoezi la upigaji kura litaanza saa sita na uhakiki mlangoni utasimamiwa na jeshi la polisi.
scout watashughulikia masuala yote ya ndani kama kubeba mabox ya kura na marufuku mgombea yoyote kusimama na kumpendekeza mgombea Fulani awe kiongozi.

No comments:

Post a Comment