KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, August 26, 2012

BANDARI YA AKINA BANKA, MESHACK ABEL NA THOMAS MOURICE KUCHEZA NA YANGA JUMATANO TAIFA.


  Timu ya bandari ya Mombasa inatarajia kufanya ziara nchini Tanzania ambapo itakuwa na michezo miwili ya kirafiki.
Timu hiyo ambayo inashiriki ligi daraja la kwanza nchini Kenya hivi karibuni iliwasajili wachezaji watatu toka nchini Tanzania akiwemo Mohamed Banka , Meshack Abel na Thomas Morice.
Akiongea na Rockersports toka Mombasa nchini Kenya kiungo Mohamed Banka amesema tayari uongozi wa Bandari umethibitisha juu ya ujio wao hapa nchini na kwamba wanatarajia kuwasili nchini jumanne tayari kwa mchezo wao wa kwanza dhidi ya Yanga jumatano kabla ya mchezo wa pili dhidi ya Coast Union ya Tanga utakao fanyika katika uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
Bandari ambayo ili wahi kumsajili huko nyuma mlinda mlango Ivo Mapunda, kwasasa inaongoza ligi daraja la kwanza nchini Kenya kwa idadi kubwa ya mabao  ikiwa imeiacha timu inayo ifuata kwa tofauti ya points 12.
Banka amesema kwasasa wamekuwa kivutio kikubwa nchini Kenya kiasi mashabiki wa soka na wapenzi wa Bandari wamekuwa wakifurika uwanjani kwenda kuangali huduma yao ndani ya klabu hiyo ambayo kimsingi mashabiki wamekuwa wakiridhika.
Banka amesema Meshack amekuwa lulu katika timu hiyo kama ilivyo kwa Thomas Morice ambaye amekuwa akipachika mabao kila anapo pata nafasi ya kufanya.

Bofya hapa kumsikiliza banka

No comments:

Post a Comment