KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, August 26, 2012

ITC ZA OCHIENG NA KINJE SASA SAFI.


Pascal Ochieng

Klabu ya Simba kukamilisha ITC za Kinje na Ochieng
Klabu ya Simba imesema iko katika hatua nzuri ya kukamilisha suala la hati ya kimataifa ya uhamisho ITC ya wachezaji wake wawili Salum Kinje na Pascal Ochieng.
Akiongea na Rockersports afisa habari wa Simba Ezekiel Kamwaga amesema wana matumaini ya kukamilisha suala hilo ndani ya masaa 48 yajayo na kwamba kwasasa kuna ujumbe wa Simba jijini Nairobi nchini Kenya unafuatilia kazi hiyo.
 Hivi karibuni shirikisho la soka nchini lilitoa orodha ya wachezaji ambao wameombewa ITC na vilabu mbalimbali nchini kutoka nje ya nchi ambapo kwa upande wa Yanga na tayari ITC zao zimepatikana ni Nizar Khalfan kutoka Vancouver Whitecaps ya Canada, Didier Kavumbagu (Atletico Olympic- Burundi) na Mbuyu Twite kutoka FC Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).
Kwa upande wa Simba ni Musa Mude (Sofapaka, Kenya) na Daniel Akuffor (Stella Abidjan, Ivory Coast) wakati Mtibwa Sugar ni Shabani Kisiga timu ya El Itihad ya Oman.
 Waliopata ITC kwa upande wa Kagera Sugar ni Wilfred Ojodale Ame na Benjamin Efe Ofuyah wote kutoka FC Abuja ya Nigeria. Wengine ni Deangelis Silva kutoka New Road ya Nepal kwenda Coastal Union, George Odhiambo kutoka Randers FC ya Denmark kwenda Mtibwa Sugar na Jerry Santo kutoka Tusker, Kenya kwenda Coastal Union.
TFF ilisema wachezaji ambao wameombewa usajili na ITC zao bado hazijapatikana ni Salum Kinje na Pascal Ochieng wa Simba kutoka AFC Leopards.
TFF imetaka klabu ambazo hazijakamilisha usajili na kupata ITC zina fursa ya kufanya hivyo hadi Septemba 4 mwaka huu ambapo dirisha litafungwa.


No comments:

Post a Comment