KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, August 27, 2012

KIMATAIFA:Afellay kuondoka Barcelona kwa mkopo,Mwamuzi anasema Coentrao alimuita mtoto wa Malaya (son of a w***e) ndiyo kisa cha kumpa kadi nyekundu,Spurs na Real Madrid wakubaliana euro milioni €37 kumuhamisha Modric,Chicharito:Raha Manchester United kumsajili Van Persie na Samuel Eto'o agoma kuichezea Cameroon.


Afellay kuondoka Barcelona kwa mkopo
Wakala wa Ibrahim Afellay , Rob Jansen, ameweka wazi kuwa mchezaji huyo wa kimataifa wa uholanzi yuko mbioni kuihama Barcelona kwa mkopo.
nyota huyo wa zamani wa PSV anaonekana kama ni mtu asiye na umuhimu kwasasa katika kikosi cha Barcelona kiasi hata kuachwa katika kikosi ambacho kiliifunga Osasuna kwa mabao 2-1 mwishoni mwa juma.
Afellay yuko mbioni kuondoka ili akatafute timu mbayo atapata nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza na mpango huo wa mkopo unaonekana kuwa ukingoni.
Jensen amenukuliwa na Studio Voetbal
"ni mchezaji mwenye kiwango cha mafanikio Barcelona, lakini kilicho mrudisha nyuma ni majeraha. Itakuwa vema kujaribu kupata sehemu ambayo atacheza. Kwasasa tuko katika mchakato kuangalia uwezekano,".
Afellay alijiunga na Barcelona akitokea PSV mwezi January 2011, lakini majeraha yamemnyima fursa ya kuonyesha uwezo msimu uliopita.
Mwamuzi anasema Coentrao alimuita mtoto wa
 Malaya (son of a w***e) ndiyo kisa cha kumpa
 kadi nyekundu.
Mwamuzi Miguel Angel Perez Lasa ameeleza juu ya maamuzi yake ya kumpa kadi nyekundu ya moja kwa moja Fabio Coentrao katika mchezo ambao Real Madrid ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-1 mchezo wa ligi ya Hispania ‘La Liga’ dhidi ya Getafe hapo jana.
amenukuliwa Perez Lasa kupitia taarifa yake ya baada ya mchezo ambayo imemnukuliwa na gazeti la Marca akisema
"kunako dakika ya 88 , mchezaji namba (5) Fabio Alexandre Da Silva Coentrao alitolewa nje kutokana na sababu ifuatayo: alikabiliana na mimi wakati mchezo ukiwa umesimama na kunitukana nilipokuwa nimesimama karibu yake na kuniita mtoto wa malaya".
Kadi hiyo haina madhara kwa mchezo wa pili wa marudiano wa Spanish Supercopa dhidi ya Barcelona, isipokuwa ni kwa michezo ligi ya Hispania La Liga.
Madrid ilifungwa mabao 3-2 katika mchezo wa kwanza Camp Nou wiki iliyopita ambapo mchezo wa marudiano utapigwa Santiago Bernabeu jumatano ijayo.
Real Madrid wamnunua Modric toka Spurs
kwa euro milioni €37
Luka Modric amefanikiwa katika vipimo vya afya vya Real Madrid na rasmi amekamilisha uhamisho wake wa ada ya euro milioni 37 kuondoka Tottenham, na ameingia mkataba wa miaka mitano na Real Madrid.
Mabingwa hao wa La Liga walikuwa wakifukuzia saini ya Modric katika kipindi chote cha majira ya kiangazi ambapo hatimaye wamefanikiwa baada ya kukubaliana na Spurs.
Uhamisho wake pia unajumuisha makubaliano ya mpango wa Urafiki "partnership agreement" ambao kimsingi unatoa fursa kwa klabu hizo mbili kubadilishana wachezaji na kocha ikiwa ni pamoja na kucheza michezo ya kirafiki.
Real Madrid imethibitisha taarifa hiyo kupitia mtandao wa klabu hiyo ikisomeka
"Real Madrid na Tottenham Hotspur wamekubaliana juu ya uhamisho wa Luka Modric, ambaye atakuwepo katika klabu hii kwa miaka mitano . vilabu vyote viwili vimekubaliana kujenga makubaliano ya ushirikiano."
Chicharito:Raha Manchester United kumsajili
Van Persie
Javier Hernandez anaangalia mwelekeo mpya wa matumaini kwa kufanya kazi na mshambuliaji Robin van Persie, huku akisisitiza kuwa ushindani katika sehemu hiyo ya ushambuliaji utaisaidia Manchester United kufanya vema.
Mashetani wekundu walilazimika kulipa pauni milioni £24 kumpata mduchi huyo ambaye aliifungia Arsenal jumla ya mabao 30 msimu uliopita kabla ya kuonyesha mahaba ya kuelekea Emirates Stadium.
Chacharito amesema siku zote amekuwa akijifunza kutoka kwa Van Persie, ambaye amefunga goli lake la kwanza akiwa na United katika mchezo dhidi ya Fulham jumamosi na anaimani ataongeza nguvu ya kikosi.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 24 alikuwa katika benchi akiaangalia bosi wake Sir Alex Ferguson akiwaadhibu Cottagers kwa mabao 3-2, huku mshambuliaji wa kimataifa wa Uholanzi na Shinji Kagawa wakisimamia sehemu ya ushambuliaji kwa kutupia nyavuni kila mmoja.
Casillas akubali kukosolewa na Mourinho
Nahodha wa Real Madrid Iker Casillas amesema yeye na wachezaji wenzake wanapaswa kuwajibika kufuatia matokeo ya jana ambayo walipigwa kqwa mabao 2-1 na , lakini amesisitiza Los Blancos can wanapaswa kujirekebisha baada ya kuanza vibaya msimu.
Madrid walikuwa wameanza vizuri baada ya bao la mapema la Gonzalo Higuain lakini wakapoteza umakini katika kipindi cha pili na kujikuta wakipigwa mabao mawili ya Juan Valera na Abdel Barrera.
Matokeo hayo yameiacha Mdrid na point moja baada ya michezo miwili points tano nyuma ya wapinzani wao wakubwa Barcelona.
Matokeo hayo yamemfanya Jose Mourinho kuwa mwenye hasira na kuwanyooshea kidole wachezaji akisema walikuwa katika kiwango cha kibaya isipokuwa hakuwa tayari kusema lolote baada ya mchezo huo.
Casillas amekubali ukosoaji huo, lakini kikubwa ni kuwa wameanza vibaya msimu kwa kuacha points nyingi kama ilivyokuwa msimu uliopita dhidi ya Levante na Racing Santander  kabla ya kurejea katika kasi ya ushindi.
Samuel Eto'o agoma kuichezea Cameroon
Samuel Eto'o amekataa kuichezea timu ya taifa ya Cameroon kama mgomo dhidi ya kile alichokielezea kama maandalizi mabaya yanayofanana na soka la ridhaa katika timu ya taifa.
Mshambuliaji huyo amejumuishwa katika kikosi kitakacho ikabili Cape Verde katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali ya mataifa ya Afrika baada ya kukamilisha kipindi cha adhabu yake ya kusimama katika timu ya taifa miezi nane.
Lakini Eto'o amesema kupitia barua yake kwenda shirikisho la soka la Cameroon kuwa yuko tayari kurejea na kwamba huo si msimamo wake wa moja kwa moja
Eto'o, ambaye ameicheza Cameroon jumla ya michezo 109 na kufunga jumla ya mabao 54 alifungiwa kucheza soka la kimataifa na nchi yake kutokana na kufanya mgomo ulitopkana na kutokulipwa kwa bonus za wachezaji baada ya michuano ya Morocco mwaka jana.
Shirikisho la soka la Cameroon liliandika taarifa kwenda kwa Eto'o, mwanasheria wake na klabu yake ya Anhzi Makhachkala kuwa adhabu ya mchezaji huyo imemalizika wiki hii.
Kufuatia taarifa hiyo kocha wa timu ya taifa Denis Lavagne alimjumuisha Eto'o katika kikosi cha wachezaji 23 kwa ajili ya kuikabili face Cape Verde September 8 ukiwa ni mchezo wa kwanza wa mzunguko wa mwisho kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika 2013.
Mshambuliaji huyo bado ameendelea kukuna kichwa kuhusiana na uongozi na usimamiaji mbaya wa timu ya taifa, hasa timu ya taifa inapo safari mwendo mrefu kutumia usafiri wa daraja la pili kwenye ndege.

No comments:

Post a Comment