Rio Ferdinand kurejea uwanjani wiki ijayo: Alex Fergsuon
Mlinzi wa
kati wa mashetani wekundu Rio Ferdinand huenda akarejea kikosi cha kwanza cha Manchester
United wiki ijayo hii ikiwa ni kwa mujibu wa Meneja wake Sir Alex Ferguson.
Mlinzi huyo
mwenye umri wa miaka 33 alikosekana katika mchezo wa ufunguzi wa msimu jumatatu
dhidi ya Everton mchezo ambao United ilifungwa kwa bao 1-0.
Ferdinand
anayesumbuliwa na groin anatarajiwa kuwa kuwepo kikosini katika mchezo dhidi ya
Southampton.
Kiungo wa
pembeni Antonio Valencia aliziba nafasi
ya ulinzi wa kulia kule Goodison Park, lakini meneja wake Sir Alex Furguson amesema
Rafael atakuwa tayari amerejea wiki ijayo.
amenukuliwa akisema
“Valencia anaweza
kucheza sehemu yoyote, Yule kweli ni mmarekani ya kusini , anapenda kucheza
soka ana nguvu na mwepesi na anaweza ku-tackle. ana weza kufanya mambo makubwa
kucheza upande wa kulia ni kwa muda tu”.
Xavi: Nataka kuendelea kuwa muhimu Barcelona
Kiungo ‘maestro’ wa Barcelona Xavi Hernandes ameweka wazi kuwa ana njaa ya kuendelea kupata mafanikio na kuendelea kuwa ni mchezaji muhimu katika klabu yake katika kampeni ya msimu wa 2012/2013 ndani ya Camp Nou.
Kiungo ‘maestro’ wa Barcelona Xavi Hernandes ameweka wazi kuwa ana njaa ya kuendelea kupata mafanikio na kuendelea kuwa ni mchezaji muhimu katika klabu yake katika kampeni ya msimu wa 2012/2013 ndani ya Camp Nou.
Xavi amesema
hana mpango wa kustaafu soka la
kimataifa kwasasa.
Kiungo huyo
mzoefu amekuwa ni sehemu ya wachezaji wa kikosi cha kwanza misimu 15 ndani ya
Catalans na anajivunia kuwa kwenye mafanikio.
amenukuliwa
akisema
"nataka
kufanya mambo kama hivyo msimu huu, kuendelea kuwa muhimu katika timu na
kushinda mataji"
ameendelea
kusema
"kiungo
huyo mchezeshaji pia amezungumzia soka la kimataifa akisema kwasasa hafikirii
kustaafu soka la kimataifa"
Xavi amecheza
jumla ya michezo 100 ya kimataifa akiwa na La Roja, akishinda mataji mawili ya
Ulaya na kombe la dunia 2010.
Liverpool yathibisha mkopo wa Sahin
Liverpool imethibitisha kufikia makubaliano na Real Madrid kumsanisha Nuri Sahin kwa mkopo wa muda mrefu baada ya zoezi la kipimo cha afya kukamilika.
Liverpool imethibitisha kufikia makubaliano na Real Madrid kumsanisha Nuri Sahin kwa mkopo wa muda mrefu baada ya zoezi la kipimo cha afya kukamilika.
Nuri Sahin
mwenye umri wa miaka 23 alijiunga na Real Madrid msimu uliopita baada ya
kuonesha kiwango katika klabu ya Borussia Dortmund ambayo ilitwaa taji la Bundesliga
msimu wa 2010-11, na kuchukua tuzo ya mchezaji wa msimu wa ligi ya ujerumani Bundesliga.
Aidha
mturuki huyo alishindwa kuonesha kuwango kizuri katika kikosi cha kocha Jose Mourinho na
kuruhusiwa kuondoka Bernabeau kwa mkopo kusaka timu atakayopata nafasi katika
kikosi cha kwanza.
Vilabu kadhaa
vya Premier League ikiwemo Arsenal, vilikuwa kwenye mawindo ya kupata huduma ya
Sahin lakini Brendan Rodgers amefanikiwa kushinda mbio hizo.
Taarifa ya Liverpool
imesema Sahin sasa atafanyiwa vipimo vya afya kule Merseyside
Rennes ya
Ufaransa imethibisha kumpata kiungo wa Aston Villa Jean II Makoun kwa mkopo wa
muda mrefu.
Mcameroon huyo
alitumika msimu katika klabu ya Olympiakos ya Ugiriki kwa mkopo lakini akili
yake ilikuwa kurejea nchini Ufaransa.
Meneja
Pierre Dreosii amenukuliwa akisema
"tulikuwa
tunatafuta kiungo mzoefu. namjua vizuri kwasababu niliwahi kumsaini nilipokuwa Lille,".
Makoun aliwasili
Rennes kama mkurugenzi akichukua nafasi ya Alexander Tettey, ambaye amejiunga rasmi
na Norwich ijumaa.
AC Milan imeendelea
kufukuzia saini ya kiungo wa Real Madrid Ricaldo Kaka na ikiwa ndio klabu yenye
nafasi kubwa kunasa saini hiyo licha ya vilabu vya Uingereza Manchester United,
Chelsea na Tottenham kutoa offer zao.
Mazungumzo yamekuwa
yakiendelea baina ya vilabu hivyo na Real Madrid,lakini Milan inaonekana kuwa
na kisu kikali zaidi kumrejesha San Siro kiungo wake wa zamani.
Taarifa
zinasema mpango wa kumpelekea Kaka aidha Spurs au Chelsea kwa mkopo umetupiliwa
mbali na sasa kigogo cha soka nchini Hispania Milan inaonekana kuwa kwenye
mwuelekeo wa kumpata kiungo mshambuliaji huyo huku mipango ya Luka Modric
ikiendelea.
Kwa kipindi
kirefu mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich amekuwa akimtamani Kaka lakini
mpango wa The Blues kujenga upya kikosi kwa kutumia vijana unakwamisha
kusajiliwa kwa wakongwe.
Alex
Oxlade-Chamberlain anasema yuko tayari kuziba pengo la Alex Song katika klabu
ya Arsenal kufuatia kuondoka kwake na kujiunga na Barcelona.
Baada ya Song
kuondoka kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £15 kuelekea kwa kigogo cha Catalan
na wakati huo huo kuna mazungumzo baina ya Arsenal na Real Madrid juu ya
kukamilishwa kwa mkopo wa Nuri Sahin, Arsenal imesalia na kiungo dhaifu ambacho
kinahitaji kuimarishwa.
Oxlade-Chamberlain
mwenye umri wa miaka 19 amesema yeye anao uwezo wa kujaza sahani na kuvaa viatu
vya Song.
Oxlade-Chamberlain
alikuwa akitumika kama winga, lakini Arsene Wenger anaamini huenda baadaye
akacheza sehemu ya kiungo ambayo alitumika katika mchezo wa ushindi wa mabao
3-0 dhidi ya AC Milan michuano ya vilabu bingwa msimu uliopita.
No comments:
Post a Comment