KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, August 26, 2012

MADA MAUGO:NGUMI ZA TANZANIA KUNA USHIRIKINA MIMI BASI.


Mada Maugo
Mwanamasumbwi machachari Mada Maugo  amesema hana mpango wa kucheza tena ngumi na mabondia wa Tanzania hata akipewa ahadi ya pesa nyingi.
Mada ametoa kauli hiyo alipokuwa akiongea na Rockersports akisema sababu kubwa ni ngumi za Tanzania kutawaliwa na mambo ya ushirikina ambayo yamekuwa yakionyeshwa na hadharani huku wadau na viongozi wakikosa njia ya kumaliza aibu hiyo.
Kwasasa anajipanga kuelekea nchini Marekani mwezi Novemba ambapo atakuwa na pambano na bondia wa huko ambaye hata hivyo hakuwa tayari kumtaja jina lake mpaka atakapo pata idhini ya mtayarishaji wa pambano hilo ambaye ni mmarekani.
Mada ametolea mfano hivi karibuni kujitokeza mambo kama hayo ambapo bondia mmoja alikwenda kupiga kambi nchini Msumbiji na kurejea nyumbani Tanzania akiwa na lundo la waganga wa kienyeji.
Amesema kwasasa malengo yake ni kucheza na mabondia wa nje na amejikita zaidi na kuangalia mapambano ya nje.
Mada Maugo amesema wakati jitihada za kupigana na matumizi ya bangi kwa mabondia wa Tanzania zikiwa zinaonekana kufanikiwa changamoto ya matumizi ya nguvu za giza imekuwa ni kubwa hivyo yeye ameona ni bora akaachana na mabondia wa nyumbani na kuelekea katika nje ya nchi.
Ametolea mfano pambano la Francis Cheka na Japhet Kaseba la hivi karibuni uwanja wa Taifa ambalo hata hivyo halikufanyika, akisema pambano hilo liligubikwa na mambo ya kishirikia ambapo inesemekana Cheka alikuwa nchini Msumbiji kwa ajili ya maandalizi ya pambano hilo wakati ambapo Kaseba alikuwa mkoni Kigoma ambaye alikuja katika pambano hilo akiwa na mashekh tayari kumdhoofisha mpinzani wake. 
BOFYA HAPA KUSIKILIZA

Japhet Kaseba
Fransis Cheka

No comments:

Post a Comment