KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, August 26, 2012

KIMATAIFA:Yanga-Mbiwa:Siwezi kusema no kuelekea AC Milan,Drogba: Nimejiunga Shanghai Shenhua kwasababu za kisoka si na pesa,Owen anaamini atapata klabu ya kucheza msimu huu,Rooney 'nje wiki nne' na nyinginezo.


Yanga-Mbiwa:Siwezi kusema no kuelekea AC Milan.
Nahodha wa Montpellier Mapou Yanga-Mbiwa ameweka wazi kuwa huenda akafikiria juu ya kuelekea AC Milan.
Nahodha huyo mwenye umri wa miaka 23 alikuwa akihusishwa na kutaka kuelekea kwa mabingwa hao mara saba wa ulaya msimu huu wa uhamisho wa kiangazi baada ya kampeni ya msimu wa 2011-12 maarufu kama ‘La Mosson’ ambapo aliiongoza timu yake kutwaa taji la Ligue 1.
Yanga-Mbiwa amesisitiza kuwa licha ya kuendelea kuwepo katika klabu hiyo lakini hakuna mazungumzo yaliyofanyika juu yangu msimu huu wa uhamisho na kwamba ataendelea kusalia kwenye kampeni ya sasa.
Mlinzi huyo wa kati mzaliwa wa Bangui amenukuliwa na Telefoot akisema,
"huwezi kusema hapana kuelekea Milan. mpaka sasa hakuna makubaliano ingawa bado nipo Montpellier,"
 "Lakini hatujui nini kimetokea katika siku za mwisho za kipindi cha uhamisho. tutaliandalia hilo. katika maisha unatakiwa kujiamini mwenyewe.
"Kama uhamisho hautafanikiwa mwaka, basi utafanyika mwakani."
 
Drogba: Nimejiunga Shanghai Shenhua kwasababu za kisoka si na pesa
 
Didier Drogba amesisitiza kuwa pesa si kitu kilicho pelekea kuamua kujiunga na Shanghai Shenhua ya Uchina baada ya kuondoka Chelsea.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Tembo wa Ivory alihamia mashariki mwezi June baada ya utumishi wake wa miaka minane Stamford Bridge na kusema kuwa mpango wake wa kuelekea huko ulikuwa wa kisoka zaidi.
Drogba anaamini bado ana mengi ya kutoa kama mchezaji akiwa China na kuongezea kuwa pengine asingepata changamoto ya kutosha endapo angeendelea kusalia Ulaya.
Amenukuliwa na Telefoot akisema
" Hii si kama dhahabu, ni maamuzi ya kisoka . Naamini ni sawa . Na ninaamini nimeleta kitu kipya katika klabu yangu.
 Drogba,ambaye kwasasa anacheza sambamba na mshambuliaji mwenzake wa zamani wa Chelsea Nicolas Anelka, amekuwa akivutia katika klabu yake baada ya kufunga jumla ya mabao manne katika jumla ya sita aliyoichezea timu hiyo mpaka sasa.
Amewakosoa wanaosema kuwa amekwenda kumalizia soka yake kabla ya kustaafu akisema hiyo ni sehemu ya maisha yake ya soka.
 
 Owen anaamini atapata klabu ya kucheza msimu huu.
 
Mshambuliaji wa zamani wa Uingereza Michael Owen, ambaye ameachwa na Manchester United msimu huu anaamini atapata klabu nyingine ya kuitumikia kabla ya kufungwa kwa kipindi cha usajili.
Owen mwenye umri wa miaka 32,aliachwa na United baada ya misimu mitatu ndani ya  Old Trafford lakini mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool, Real Madrid na Newcastle anasema ana matumaini anaweza kupata nafasi katika moja ya timu za ligi kuu ya nchini Uingereza Premier League.
Amenukuliwa na BBC Radio akisema,
"katika hali ya aina hii kuna mengi ambayo yanaweza kutokea baadaye kwa kuwa watu bado wanaviangalia vikosi vyao na mambo kama hayo.
"Kwa hiyo, ndiyo nimekuwa na mawasiliano na vilabu vichache lakini naamini nitapata jezi nyingine hivi karibuni "
Rooney 'nje wiki nne'
 
Mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney anakabiliwa na uwezekano wa kuwa nje ya uwanja kwa wiki nne baada ya kupata mchubuko mkubwa paja katika mchezo wa jana dhidi ya Fulham ambao United ilishinda kwa mabao 3-2.
Inavyoonekana mshambuliaji huyo huenda akakosa michezo kadhaa ya klabu yake na kimataifa wakati huu ambapo England ikiwa na michezo miwili ya kimataifa dhidi ya Macedonia na Ukraine mapema mwezi September, lakini pia klabu yake United ikitaraji kucheza dhidi ya Southampton, Wigan na Liverpool mwezi ujao.
Rooney alitolewa uwanjani zikiwa zimesalia dakika 20 alikumbana na dhoruba hiyo wakati akikabiliana na Hugo Rodallega na kulazimika kubebwa kwenye machela wakati akijaribu kuzuia mpira ndipo ‘njumu’ za mshambuliaji wa Fulham zikamparua pajani.
Meneja wake Sir Alex Ferguson amethibitisha baada ya mchezo kuwa Rooney atahitaji kupata matibabu ambayo yatamuweka nje ya uwanja katika kipindi cha mwezi mmoja.
Akiongea na Sky Sports amesema,
"Ni mchubuko mbaya . amepelekwa Hospitali na atakuwa nje ya uwanja baada ya wiki nne,"
Katika mchezo huo , Fulham ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao dakika ya tatu kupitia kwa Damien Duff.
United ikajibu kwa mabao matatu ya kipindi cha kwanza kupitia kwa Robin van Persie, Shinji Kagawa na Rafael.
Kujikanganya kwa David de Gea na Nemanja Vidic kulipelekea mlinzi wa kati Vidik kujifunga na kuandika bao la pili kwa Fulham zikiwa zimesalia dakika 25 kabla ya mchezo huo kumalizika.
Rais wa Santos anasema Ganso lazima akubali kuzomewa na mashabiki
Rais wa klabu ya Santos ya nchini Brazil Luis Alvaro de Oliveira Ribeiro amesema ni lazima nyota wa kimataifa wa Brazil Ganso akubali kuzomewa na mashabiki wa Santos kufuatia kauli yake kuwa angependelea kuvaa jezi ya Sao Paulo, ambao ni wapinzani wao wakubwa katika soka la Brazil wenye maskani yao pande za Peixe.
Katika mchezo ambao Santos walishinda kwa mabao 2-1 dhidi ya Palmeiras usiku wa jana mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 alikuwa akizomewa muda ikiwa ni hasira za mashabiki kujibu kauli yake.
Rais wa klabu hiyo Luis Alvaro de Oliveira Ribeiro amesisitiza kuwa ndio watu wa kwanza na hiyo ndiyo ilikuwa salamu zao kwa Ganso na anapaswa kukubali hilo.
Ribeiro amenukuliwa na Lancenet akisema
"Mashabiki lazima waheshimiwe . kama msanii anapanda jukwaani lazima akubali kuzomewa au kushangiliwa. Na katika soka ni hivyo hivyo, hiyo ndiyo kawaida" .
 "Mshabiki walifuata na walikuwa na kasira kufuatia kauli ya mchezaji huyu."
Ganso mwenyewe amejibu kauli ya Rais wake Ribeiro akisema Rais wake hakupaswa kutoa maneno hayo lakini amesisitiza kuwa ataendelea kutoa huduma katika klabu hiyo.
 
 Serikali ya Malawi yafunga uwanja wa Taifa kwasababu za kiusalama
 
Serikali ya Malawi imeufunga uwanja wa taifa wa nchi hiyo ulioko Blantyre miundo mbinu ya uwanja huyo kuwa mibovu pamoja na hofu ya usalama.
Waziri wa michezo wa Malawi  Enock Chihana ana matumaini kuwa Kamuzu stadium utakuwa tayari kutumika kwa ajili ya mchezo wa pili wa marudiano kati ya Malawi dhidi ya Ghana kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika 2013 mchezo ambao umepangwa kufanyika October 14.
Amenukuliwa Chihana akisema
"tuna matumaini kuwa mambo ya msingi ikiwa na ukarabati  pamoja na vifaa muhimu vya kiusalama yatakamilishwa ndani ya wakati kabla ya mchezo huo"
Amesema Kinga ni bora kuliko tiba na hi hivyo serikali tumeliona hili kwa mustakabi wa watu wetu na si vizuri kupeleka michezo yetu katika uwanja huru kama Zambia.
Serikali kwa kushirikiana na chama cha soka cha Malawi  (Fam) wamesema wana matumaimni ya kumaliza tatizo hilo haraka iwezekanavyo.
Naye Rais wa Fam, Walter Nyamirandu ameeleza juu ya kufungwa kwa uwanja huo akisema ni pigo lakini ni hatua muhimu kwa faida ya mashabiki wa soka na Malawi yenye kama nchi.
Kufungwa kwa uwanja huo kumekuja wakati ambapo kunatarajiwa kufanyika kwa fainali ya Presidential Cup kati ya Big Bullets na Moyale Barracks ambayo ilikuwa imepangwa kufanyika hii leo na sasa mchezo huo umepangwa kufanyika September 1.
Fainali hiyo imehamishiwa Civo Stadium ulioko katika mji mkuu wa Malawi, Lilongwe.
Fifa imekuwa ikitoa tahadhari kwa Malawi kupunguza uwezo wa watazamaji katika uwanja huo kutoka 60,000 mpaka  32,000.

No comments:

Post a Comment