Hatimaye Vilabu
vya Simba na Yanga vimekubali kushiriki michuano ya BancABC super8
iliyotambulishwa hivi karibuni mbele ya waandishi wa habari.
Michuano hiyo
mpya ambayo hapo kabla iliingia katika utata mkubwa juu ya kukubaliwa kwake na
vilabu hivyo vikubwa hapa nchini kutokana na kutokueleweka vizuri juu ya
maslahi yao ikiwemo suala zima la zawadi mbali na wao kama vilabu watapata nini
katika ushiri wao.
Wakiongea
kwa nyakati tofauti na Rockersports mara baada ya kikao kilichoitishwa na TFF
kuzungumzia juu ya hilo hii leo, viongozi wa vilabu hivyo viwili makamu
mwenyekiti wa Simba Geofrey Nyange Kaburu na katibu wa Yanga John Celestine
Mwesigwa wamesema kilichokuwa kinawapa tabu ni nini kilichomo ndani ya mkataba
huo ambao uliingiwa baina ya TFF na BancABC kwa faida ya vilabu hivyo shiriki.
Makamu
mwenyekiti wa Simba Kaburu amesema suala kubwa sio kukubali au kukataa kucheza katika ligi hiyo ndogo ya Super8
bali wao kama wadau hawakupata nafasi ya kuhusishwa wakati wa kuingia huo
mkataba lakini sasa wamefikia makubaliano baada ya kuambiwa juu ya masuala ya
msingi waliyokuwa wanayahitaji lakini wao pia wametoa angalizo juu ya
maandalizi yao ya ligi kuu ya Vodacom kuvurugwa na ratiba ya mashindano hayo.
Amesema wao
kama Simba kimsingi wamekubali kucheza katika ligi hiyo lakini watawatumia
wachezaji wao wa kikosi cha pili cha under
20 wakiwachanganya na wachezaji wao wapya waliosajili msimu huu na wale
ambao wanafikiria kuwasajili.
Kuhusu suala
la zawadi Kaburu amesema kimsingi wamekubali zawadi itolewe kwa bingwa pekee
lakini kuna mambo mengine muhimu wamekuwa bado wanajadiliana na TFF ambayo
yatatolewa ufafanuzi na TFF baada ya kujadiliana na wadhamini wa ligi hiyo
BancABC.
Kwa upande
wao mabingwa wa kombe la kagame Yanga kupitia kwa katibu wao Mwesigwa Celestine
wamesema wamekuwa wakiendelea na mjadala na TFF na mazungumzo yao na TFF
yanaendelea vizuri.
Amesema
kimsingi watafikia muafaka juu ya hilo kwa kuwa mjadala umefikia katika hatua
nzuri na taarifa itatolewa juu ya nini kimefikiwa baina ya pande zote tatu
yaani TFF,BancABC na vilabu vyote.
Hata hivyo
hakuwa tayari kuzungumzia ni wachezaji gani watakao watumia katika ligi hiyo
mpya
TFF
imezitaja timu za Tanzania bara za Simba,Yanga na Azam kama timu zilizoshika
nafasi za juu katika msimu uliopita wa ligi kuu ya Vodacom pamoja na timu moja
iliyopanda daraja la kwanza kushiriki ligi hiyo ambapo watakuwa wakiungana na
vilabu vya Zanzibar vyenye matokeo yanayo fanana na hayo.
Michuano
hiyo ya BancABC SUP8R soccer Tournment 2012 imepangwa kwa mtindo wa makundi mawili
na itachezwa kwenye miji ya Dare s salaam, Mwanza , Arusha na Zanzibar na
imepangwa kuanza August 4.



No comments:
Post a Comment