KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, November 2, 2012

MUDA MFUPI UJAO MESSI KUITWA BABA AYAPOTEZEA MAZOEZI YA BARCA, ARSEN WENGER ANASEMA HAFIKIRII KULIPIZA KISASI CHA BAO 8-2 TOKA KWA MAN UNITED NA BARANI AFRIKA AL HILAL KUMALIZA KADHIA YA KUTINGA FAINALI.

Lionel Messi akifuatana na mpenzi wake Antonella Roccuzzo muda mfupi kabla ya kujifungua.
Hospitali aliyopelekwa Antonella Roccuzzo mpenzi wake Messi kwa maandalizi ya kujifungua
Hapa wakila raha kabla ya ujauzito

Messi ayapotezea mazoezi ya Barcelona akimsubiri mtoto wake wa kiume Thiago mtarajiwa.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Argentina na klabu ya Barcelona Lionel Messi masaa machache yajayo anatarajia kutwa baba kufuatia mpenzi wake ambaye ni mja mzito kukimbizwa hospitali kwa ajili ya kujifungua.

Nyota huyo amepewa ruhusa na klabu yake na kuachana na mazoezi ya leo kwenda kuungana na mpenzi wake Antonella Roccuzzo kumsibiri kwa hamu mtoto wao wa kiume aliyepewa jina tayari la Thiago.

Roccuzzo amepelekwa katika hospitali ya USP Dexeus mapema asubuhi ya leo na nyota Lionel Messi kujiunga naye katika hospitali hiyo iliyokaribu na Camp Noun na hivyo kukosa mazoezi ya leo.

Kocha wa Barca Tito Vilanova amesema bado haja amua kama Messi atakuwepo katika mchezo wa kesho wa ligi ya soka nchini Hispania maarufu kama ‘Primera Division’ dhidi ya Celta Vigo kama mpenzi wake atafanikiwa kujifungua muda mfupi ujao kabla ya mchezo.


Wenger sina nia ya kulipiza kisasi cha mabao 8-2 kwa United.

Meneja wa Arsenal  Arsene Wenger amesema kamwe hana nia ya kulipiza kisasi kichapo alichokipata ambacho si rahisi kusahau toka kwa mashetani wekundu katika mchezo utakao pigwa cha kuvumilika mwishoni mwa juma hili.

Washika mitutu hao walipata kichapo takatifu cha mabao 8-2 toka kwa Manchester United msimu uliopita kichapo ambacho kiliibua maswali mengi juu ya hatma ya Wenger na sasa anaingia katika mchezo huo huku maswali yakiibuka juu ya uwezo wa safu yake ya ulinzi.

Safu ya ulinzi ya Arsenal iliruhusu mabao manne ndani ya dakika 37 za mchezo wa kombe la ligi (siku hizi Capital One) dhidi ya Reading mchezo uliofanyika jumanne huku pia rikodi ya meneja hiyo baada ya michezo kumi na moja ikionekana kuwa ina mashaka.

Mwenyewe amenukuliwa akisema
"hiyo ni takwimu tu kuhusu mimi lakini tunakwenda katika mchezo huo tukiwa tunajiani sana"
"siwezi kuzungumzia matokeo ya mchezo wa msimu uliopita wakati tukielekea katika mchezo wa kesho ukizingatia kuwa karibu asilimia tisini ya wachezaji watakao kuwepo kesho walikuwepo walicheza katika mchezo wa msimu uliopita kule Old Trafford.

"ni kweli kuna hisia za kimatokeo kama hivyo lakini suala la kulipiza kisasi si jambo ninalo lifikiria katika mchezo huo. Kisoka hilo la matokeo ya aina hiyo si muhimu sana.

"suala la ulinzi wakati wa mchezo si jibu la udhaifu wa kikosi , lakini pia uwezo wa mpinzani pia. Unatakiwa kupongeza kama una ubora katika sehemu ya ulinzi katika katika ligi na ninachoweza kuahidi ni kwamba tumeifanyia kazi safu yatu ya ulinzi.

Wenger anaamini kikosi chake kinaweza kuyaleta matokeo ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya wapinzani wao wa kutoka London ya kaskazini Tottenham katika mchezo wa ligi uliopita mpaka Old Trafford watakapo kuwa wakikabiliana kwa mara ya kwanza na mshambuliaji wake wa zamani uso kwa uso Robin van Persie tangu ajiunge na United msimu huu akitokea Arsenal.


Esperance kumkosa Msakni anasumbuliwa na mguu

Esperance itakuwa dimbani bila ya nyota Youssef Msakni katika mchezo wa kwanza wa fainali ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Al Ahly mchezo utakao pigwa hapo kesho.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wsa miaka 21 alifanyiwa upasuaji hapo jana baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa ‘appendicitis’ na hivyo hatakuwepo katika kikosi kitakacho elekea nchini Misri.

Kukosekana kwake ni pigo kubwa kwa watunisia hao ambao wamedhamiria kutetea taji hilo walilolitwaa msimu uliopita.

Msakni ameifungia Esperence jumla ya mabao manne katika michuano hiyo msimu huu.
Aidha  Esperance tayari imeshakubali kumuuza mshambuliaji huyo baada ya mchezo wa fainali ambapo inaarifiwa kuwa mchezaji huyo ameridhia kujiunga na Lekhwiya ya nchini Qata mwezi January mwakani.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Tunisia ni miongoni mwa wachezaji ambao wametajwa kuwania tuzo ya mwanasoka bora barani Afrika.

Al Hilal kumaliza nuksi ya kuishia nusu fainali kombe la shirikisho

Al Hilal ya Sudani inatarajiwa kumaliza balaa la kuishia katika hatua ya nusu fainali ya kombe la shirikisho barani Afrika ambapo hii leo watakuwa wenyeji wa Djoliba ya Mali katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali.

Ndani ya kipindi cha miaka mitano Hilal imepoteza mara tatu katika ligi ya mabingwa Afrika na kuishia katika hatua ya nusu fainali na mara moja katika kombe la shirikisho.

Klabu hiyo ya nchini Sudani ilimaliza katika nafasi ya pili katika kundi A na ikijikuta ikicheza na mshindi wa kundi la B Djoliba ya Mali.

AC Leopards itakuwa mwenyeji wa Al Merreikh katika mchezo wa nusu fainali nyingine utakapigwa jumapili.
Baada ya kuhaha katika miaka ya hivi karibuni , Hilal itataka kutumia faida ya uwanja wa nyumbani kupata matokeo ya kushiba kabla ya mchezo wa pili wa marudiano utakao pigwa wiki mbili zijazo nchini Mali.

Hilal, ambayo imesheheni nyota kibao kutoka mataifa ya Cameroon, Equatorial Guinea, Mali, Nigeria, Senegal na Zimbabwe, iliwachapa wa-Mali wengine kule Bamako katika mchezo wa ‘play-off’ na kutinga hatua ya makundi.

Wakiongozwa na kocha raia wa nchi mbili Ufaransa na Italia Diego Garzitto, Hilal ilisonga mbele katika hatua ya makundi mpaka hatua ya nusu fainali baada ya kupata matokeo ya ushindi michezo minne, sare mbili na kupoteza mchezo mmoja.

Mshambuliaji raia wa Zimbabwe Edward Sadomba amekuwa chachu ya ushindi ya timu hiyo akifunga mabao matano mwaka mmoja baada ya kumaliza akiwa mfungaji bora kwa kufunga magoli saba katika ligi ya mabingwa msimu uliopita.

Djoliba imeingia hatua hiyo baada ya ushindi wake wa nyumbani na ugenini dhidi ya mshindi wa pili bingwa wa michuano ya vilabu bingwa mwaka jana 2011 Wydad Casablanca.


No comments:

Post a Comment