KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, December 12, 2012

Gomez: kutwaa taji la Bundesliga ndio kila kitu si yeye kucheza na Pazzini awataka AC Milan wasibweteke na ushindi mfululizo.



Mshambuliaji wa Mario Gomez amesema kwake yeye kusugua benchi sio tatizo,  fahari yake ni kuona Bayern Munich inatwaa taji la Bundesliga mwisho wa msimu.

Mshambuliaji huyo amekuwa akisugua benchi baada ya kupata majeraha tangu siku za mwanzo za kuanza msimu msimu wa 2012-13 lakini amesisistiza hilo si tatizo kikubwa ni kutwaa taji kuliko kurejea katika kikosi cha kwanza.

Amenukuliwa na gazeti la Bild akisema

"ki ukweli lengo langu kubwa ni kushinda taji la Bundesliga. Mambo mengine si muhimu kuliko taji".

Gomez ameshinda mataji mawili mpaka sasa akianza kupata taji msimu wa 2006-07 akiwa na Stuttgart na baadaye akiwa na Bayern msimu wa 2009-10.



Pazzini: AC Milan inabidi ikaze buti

Giampaolo Pazzini amesisitiza kuwa AC Milan inabidi kuongeza uwezo wake wa kiuchezaji katika wiki za hivi karibuni ili kupunguzo kupoteza michezo kama ilivyokuwa katika miezi ya mapema ya kuanza ligi msimu huu wa 2012-13.

Milani imekuwa ikifanya vizuri katika mfulilizo wake wa michezo saba ya ligi kuu ya Italia ‘Serie A’ katika siku za hivi karibuni, lakini Pazzini ameonya hiyo isiwe kigezo cha kubweteka na matokeo hayo katika sehemu iliyosalia ya msimu

Amenukuliwa na Sky Sport Italia akisema

"tulianza vibaya na morali ilikuwa chini na matokeo hayakuwa mazuri"

Milan watarejea katika mfululizo wa michezo ya Serie A nyumbani dhidi ya Pescara jumapili.


No comments:

Post a Comment