Rais wa Barcelona
Sandro Rosell amesema mlango bado uko wazi kwa Victor Valdes endapo mlinda
mlango huyo atabadili mawazo yake kuamua kusaini mkataba mpya na klabu yake hiyo.
Mapema mwezi
huu Valdes aliiambia klabu hiyo kupitia wakala wake kuwa hafikirii kuomgeza
mkataba mwingine na Barca baada ya mkataba wake kumalizika june 2014.
Taarifa za
mwendelezo zinasema kuwa Barca imekuwa katika mipango ya kufanya usajili mkubwa
wa kuziba pengo lake ambapo wamekuwa wakihusishwa na kuwataka walinda mlango wa
Liverpool Pepe Reina, David De Gea wa
Manchester United,Marc-Andre ter Stegen wa Borussia Moenchengladbach, Vicente
Guaita wa Valencia na Thibaut Courtois ambaye kwasasa yuko kwa mkopo Atletico
Madrid.
Kocha wa Barcelona
Tito Vilanova na baadhi ya wachezaji kama Andres Iniesta na Lionel Messi wamekaririwa
wakisema wanaheshimu maamuzi ya Valdes lakini wanaamini mlinda mlango huyo
huenda pia akaamua kusalia katika klabu hiyo.
Katika mchezo
wa jumapili ambapo Barca ilishinda 5-1 dhidi ya Osasuna katika dimba la Camp
Nou mashabiki walionekana kumpa tano mlinda mlango huyo na kumkubali zaidi
tangu alipotoa tamko lake la kusitisha kuongeza mkataba mwingine baada ya kumaliza
mkataba wa sasa.
Valdes alijiunga
na Barca akiwa kijana mdogo mwaka 1992 na amekuwa na klabu hiyo wakati wote na
hakuwahi kutoa tamko lolote la kutaka kuihama klabu hiyo kabla ya katikati ya mwezi
huu kupitia wakala wake ambapo alitoa tamko ambalo limeonekana kupingwa na
wengi
No comments:
Post a Comment