Manchester
United imetenga pauni pauni milioni £8 kwa ajili ya kumnasa kiungo wa Celtic
na timu ya taifa ya Kenya Victor Wanyama kabla ya kufungwa kwa dirisha dogo la
usajili.
Licha ya
kwamba Celtic inaonekana kutokuwa tayari kumtoa kiungo huyo kwa kuwa bado ni
muhimu kwao kutokana na ukweli kwamba alifunga goli goli muhimu la ushindi wa
nyumbani katika mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Barcelona, bado United
inaonekana kudhamiria kunasa saini ya kiungo huyo.
Uwezo wa
Wanyama umevutia vilabu mbalimbali katika miezi ya hivi karibuni na vilabu
vingi vinaonekana kufungua mazungumzo na mabingwa hao wa soka wa ligi ya
Scotland na mchezaji mwenyewe huku United wakionekana kuwa tayari kufanya hivyo
kwasasa.
Sir Alex
Ferguson alimuona Wanyama wakati wa mchezo ambao Celtic ilishinda kwa mabao 4-0
katika dimba la nyumbani dhidi ya Dundee United wiki iliyopita.
Kama hiyo
haitoshi kinachoonekana sasa ni kwamba kiungo huyo anaangaliwa kama kama chaguo
muhimu la kuziba nafasi ya mchezaji mwingine mlengwa ambaye mipango ya United kunasa imeonekana kushindwa, huyu si mwingine
bali ni kiungo wa PSV Eindhoven Kevin Strootman.
No comments:
Post a Comment