KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, March 5, 2013

Klitschko aweka rehani mataji yake yote dhidi ya mtaliano Pianeta.

Wladimir Klitschko atatetea mataji yake ya uzito wa juu ya WBA, IBF na WBO dhidi ya swahiba wake wa zamani wa mazoezi Francesco Pianeta pambano ambalo litachezwa huko Mannheim May 4.
Klitschko, raia wa Ukraine mwenye umri wa miaka 36 atakuwa anatetea kwa mara ya 14 akiwa ubingwa wa dunia wa uzito wa juu.
Pianeta, ambaye ni raia wa Italia lakini maskani yake yakiwa nchini Ujerumani hajapoteza hata pambano moja katika mapambano yake 29 aliyocheza mbali ya kwenda sare pambano moja.
Amenukuliwa Pianeta akisema
"Wengi wanadhamni mimi nitapigwa, lakini ukweli ni kwamba nitamgonga Klitschko na kuugeuza ulimwengu wa masumbwi."

No comments:

Post a Comment