KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, March 5, 2013

NDOTO ZA VIDIC NI KUCHEZA NA CHRISTIANO RONALDO TENA UNITED.

 Nahodha wa Manchester United Nemanja Vidic anaamini kuwa iko siku mshambuliaji wa zamani wa United Cristiano Ronaldo atarejea Old Trafford.
Ronaldo usiku huu atakuwa akirejea kwa mara ya kwanza  Old Trafford akiwa na kikosi cha Real Madrid ambacho kitakuwa kikikabiliana na kikosi chake cha zamani United katika mchezo wa ligi ya mabingwa barani Ulaya hatua ya 16 bora.
Vidic, ambaye amecheza na mreno Ronaldo kabla ya kuihama kwa uhamisho wenye thamani ya rekodi ya dunia wa pauni milioni £80 na kujiunga katika viunga vya Bernabeu mwaka 2009, ana matumaini kuwa yeye na mshambuliaji huyo iko siku wataungana tena na kucheza pamoja chini ya meneja babu Sir Alex Ferguson.

No comments:

Post a Comment