KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, March 25, 2013

SERGIO BUSQUETS ANA WASIWASI NA TAIFA KUBWA HISPANIA KUSHINDWA KWENDA BRAZIL. na CRISTIANO RONALDO KUELEKEA AZERBAIJAN LICHA YA ADHABU YA KUSIMAMA MCHEZO MMOJA.




Sergio Busquets amesema taifa kubwa linaelekea kushindwa kufuzu kwa ajili ya fainali ya kombe la dunia 2014 wakati huu ambapo kikosi cha Vicente del Bosque kikiwa katika maadnalizi kukutana dhidi ya Ufaransa mchezo mgumu kabisa ambao utapigwa katika jiji la Paris.

Kufuatia Ufaransa kushinda dhidi ya Georgia na kisha Hispania kwenda sare dhidi ya Finland ijumaa iliyopita, mabingwa hao watetezi wa taji wamejiweka pabaya katika msimamo wa kundi I wakiwa nyuma kwa alama mbili toka kwa Ufaransa maarufu kama Les Bleus.

Licha ya kwamba watakuwa wamesaliwa na michezo mitatu mara baada ya mchezo wa Paris, bado majaaliwa ya kufuzu yatategemea na nani atakae kuwa amekalia usukani wa kundi lakini nafasi ya upendeleo ya moja kwa moja kwa ajili ya fainali hizo.

Kiungo wa Barcelona Busquets mwenye umri wa miaka 24 anatarajiwa kushika dimba la Hispania baada ya matokeo ya sare ya mwezi Oktoba mjini Madrid ambapo anasema anamatumaini kuwa kikosi hicho cha Didier Deschamps hakiwanyimi usingizi kuelekea mchezo wa Jumanne.

Akiongea na Le Parisien amesema
"Timu nyingi zinabadilisha mbinu za uchezaji dhidi yetu" wakati mwingine inakuwa ni kama kukamiana”

Vilanova kurejea Barcelona baada ya kansa nchini Marekani.
 Kocha wa Barcelona Tito Vilanova anatarajia kurejea nyumbani wiki hii baada ya mwezi mmoja wa matibabu ya kansa inayomsumbua.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 44 alikuwa akipatiwa matibabu jijini New York nchini Marekani baada ya kugunduliwa kuwa bado anasumbuliwa na tezi zenye madhara ya kusababisha kansa baada ya kufanyiwa uchunguzi mwezi Desemba.

Msaidizi wake Jordi Roura, amekuwa akishikilia nafasi yake ambapo taarifa ya klabu hiyo kupitia mtandao wa klabu hiyo imesema kurejea kwake haimaanishi kuwa atakuwa anarejea moja kwa moja katika benchi la ufundi la klabu hiyo.

Michezo ijayo ya Barcelona watakuwa wakikabiliana dhidi ya Celta Vigo jumamosi ukiwa ni mchezo wa ligi kuu ya nchini Hispania kabla ya mchezo wa Jumanne dhidi ya Paris Saint-Germain mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya.

Vilanova amekuwa karibu na klabu yake hiyo katika kipindi chote alichokuwa hayupo ambapo amekuwa akifuatialia mazoezi kupitia njia ya TV na kuwasiliana na benchi la ufundi wakati wa michezo mbalimbali kwa njia ya simu.

Ronaldo kwenda Azerbaijan licha ya kuwa na kadi mbili za njano.
 Nahodha wa timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo anatarajiwa kuelekea Azerbaijan pamoja na kikosi kizima cha timu hiyo kwa ajili ya mchezo wa Jumanne wa kuwani kufuzu kwa fainali ya kombe la dunia licha ya kwamba mshambuliaji huyo kwasasa anatumikia adhabu ya kusimama mchezo mmoja.

Mshambuliaji huyo wa Real Madrid alikuwepo ndani ya dakika zote 90 za mchezo uliopita dhidi ya Israel mchezo uliofanyika Ijumaa na kumalizika kwa matokeo ya sare ya mabao 3-3 lakini alijikuta akiadhibiwa kwa kadi ya pili ya njano baada ya kucheza ndivyo sivyo na hivyo kuukosa mchezo huo huko Baku.

 Hali hiyo inaweka uwezekano wa kurejea kwake mapema katika jiji la Madrid kujiandaa na mchezo wa ligi dhidi ya Real Zaragoza na baadaye kuelekea katika mchezo dhidi ya Galatasaray ukiwa ni mchezo wa ligi ya mabingwa katika dimba la Santiago Bernabeu April 3.

No comments:

Post a Comment