KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, March 25, 2013

TENGA AWAPONGEZA WACHEZAJI, SERIKALI NA TENGA KUFUNGUA SEMINA ELEKEZI COPA COCA COLA.



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga
ameipongeza wachezaji wa Taifa Stars na benchi lao la ufundi,
washabiki, mdhamini na Serikali kwa kufanikisha ushindi wa jana.
Tenga amesema ushindi huo umetokana na ushirikiano kutoka kwa wadau
wote, na hasa wachezaji walioonesha kiwango kikubwa kulinganisha na mechi zilizopita ikiwemo kiwango cha kujituma uwanjani.
Amesema Serikali ni mdau mkubwa wa mpira wa miguu katika miundombinu, usalama na idara zake mbalimbali ikiwemo Uhamiaji ambayo imefanikisha kwa kiasi kikubwa kuwepo kwa mechi hiyo ambapo Taifa Stars iliifunga Morocco mabao 3-1.

Katika hatua nyingine.
 

TENGA KUFUNGUA SEMINA ELEKEZI COPA COCA COLA

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga
atakuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa semina elekezi ya michuano ya
Copa Coca Cola itakayofanyika kesho (Machi 26 mwaka huu).

Semina hiyo inayoshirikisha makatibu wakuu wa vyama vya mpira wa miguu
mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar itafanyika Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam na itafunguliwa na Rais Tenga kuanzia saa 3 kamili asubuhi.

Washiriki wengine katika semina hiyo itakayokuwa na watoa mada kutoka
TFF na wadhamini kampuni ya Coca Cola ni waratibu wa michuano ya Umoja
wa Michezo wa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA).

No comments:

Post a Comment