KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, August 5, 2013

Gervinho & Marouane Chamakh waonyeshwa mlango wa kutokea Arsenal, Manchester United yakataa ombi la pili la Chelsea kumtaka Rooney na Brendan Rodgers anasema Arsenal wanacheza ngoma ya kujifurahisha kuhusu Suarez .


 Taarifa zinasema kuwa Gervinho na Marouane Chamakh wanakaribia kukamilisha uhamisho wao wa kuondoka katika klabu yao ya Arsenal, hii ikiwa ni kwa mujibu wa meneja wa washika bunduki  Arsene Wenger.

Mshambuliaji wa kimataifawa Ivory Coast Gervinho, ambaye alijiunga na washika mitutu hao kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £11 akitokea Lille mwaka 2011, aliwasili nchini Italia Jumapili kumalizia mipango yake ya kujiunga na ligi ya nchi  hiyo inayojulikana kama Serie A katika klabu ya Roma kwa ada iliyoripotiwa kuwa ni pauni milioni £6.9.

Kwa upande wake Chamakh, ambaye alihamia klabu hiyo akitokea katika klabu ya Bordeaux mwaka 2010, anajipanga na kujiunga na Crystal Palace, licha ya kwamba bado haijaamuliwa endapo uhamisho wake utakuwa ni wa mkopo au wa minajili ya kudumu.

Wote wamekuwa lawamani ndani ya klabu hiyo kutoka pande za London ya kaskazini kwa kutokuwa katika ubora wa kuwepo katika kikosi cha kwanza.

Gervinho mwenye umri wa miaka 26, alifunga jumla ya magoli 11 katika jumla ya michezo 63 atakuwa akijiunga na bosi wa Roma Rudi Garcia, ambaye alikuwa naye katika klabu ya Lille.



Baada ya kuichezea West Ham kwa mkopo msimu uliopita ,Chamakh alishindwa kushawishi kurejea kwa washika mitutu  na sasa safari yake ikiwa ni Palace ambao anaonekana kama ndiye mwenye thamani ya juu katika usajili wa klabu hiyo majira ya kiangazi.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 29 alifunga jumla ya magoli 11 katika msimu wa kwanza ndani ya Arsenal lakini alishindwa kuendeleza ubora wake ndani ya klabu hiyo baadaye.

Kikosi cha mzee Wenger kilibanjuliwa mabao 2-1 na Galatasaray Jumapili huku mshambuliaji wa zamani wa Chelsea Didier Drogba akifunga magoli yote huku kikosi hicho kikitokea nyuma kimatokeo.

Mpaka sasa Arsenal imefanikiwa kufanya usajili wa mchezaji mmoja tu mwenye umri wa miaka 20 raia wa Ufaransa mshambuliaji Yaya Sanogo kwa uhamisho huru akitokea Auxerre.

 Wayne Rooney: Manchester United yakataa ombi la pili la Chelsea kumtaka Rooney.

Manchester United imeitupia mbalia ofa kutoka katika klabu ya Chelsea kwa ajili ya mshambuliaji wa kimataifa wa England Wayne Rooney.

Ombi hilo lilifanywa usiku wa jana ambayo ilikuwa na thamani ya pauni milioni £25 lakini United imeendelea kung’ang’ania msimamo wake kuwa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 hauzwi.

Rooney, ambaye amekuwa akiendelea kutaka kuondoka United, aliameachwa kueleka katika mchezo wa kesho usiku Jumanne katika safari ya michezo ya kujiandaa na msimu huko Stockholm akiarifiwa kuwa ana matatizo ya bega.

Imefahamika kuwa mshambuliaji huyo alipatwa na dharuba wakati wa mchezo usiokuwa na mashabiki dhidi ya Real Betis Jumamosi.

Chelsea ilianza kuweka ombi la kumtaka Rooney kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £20 ambayo ilipigwa chini mwezi uliopita wamerejea tena na ombi la pili kwa kuongeza dau lao.

Meneja wa United David Moyes ameendelea kusisitiza kuwa  Rooney atasalia kwa mabingwa hao wa England huku meneja wa Chelsea Jose Mourinho akiendelea kudhania kumpeleka darajani Stamford.


Luis Suarez: Brendan Rodgers anasema Arsenal wanacheza ngoma ya kujifurahisha kuhusu Suarez
 Bosi wa Liverpool Brendan Rodgers anasema klabu ya Arsenal ni kama inajifurahisha katika jaribio lao la kutaka kumsajili mshambuliaji wake Luis Suarez.

Liverpool imeipiga chini ofa ya rekodi ya Arsenal ya pauni milioni £40 na ziada ya pauni milioni  £1, jumla yake ambao inaonekana ni kama itawezesha kuvunja mkataba wa Suarez.

Liverpool inasema ofa ya Arsenal kwa mshambuliaji huyo ni ya chini kwa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26.

Suarez ambaye alifunga jumla ya magoli 30 msimu uliopita alijiunga na wekundu hao mwaka 2011 akitokea Ajax kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £22.7 na ana mkataba wa nyongeza alioingia na klabu yake Agosti 2012.

Liverpool pia imefanya maombi mengine ikiwa ni pamoja na kumtaka mshambuliaji wa Atletico Madrid Diego Costa kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £21 pamoja na hayo bado Rodgers ameendelea kusisitiza kuwa hana nia ya kumuuza Suarez.



No comments:

Post a Comment