KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, August 5, 2013

Wachezaji wa Ujerumani walitumia dawa za kuongeza nguvu.

Ripoti ya uchunguzi kwamba iliyokuwa Ujerumani ya Magharibi iliendesha mipango ya matumizi ya dawa zilizopigwa marufuku michezoni katika miaka ya 1970, ikiungwa mkono na serikali, imechapishwa.

Mradi uliofadhiliwa na serikali wa dawa za kuongeza nguvu mwilini pia ulitumiwa katika iliyokuwa Ujerumani ya Mashariki, lakini ripoti ya utafiti uliofanywa na jopo kutoka chuo kimoja kikuu mjini Berlin pia imesema kiwango cha matumizi ya dawa hizo kilikuwa cha kutisha katika iliyokuwa Ujerumani ya Mashariki.

Kwa kuzingatia mahojiano yaliyofanywa na zaidi ya mashahidi 50, timu kutoka chuo kikuu cha Humboldt kilitumia miaka mitatu kufanya utafiti wa ripoti yenye kurasa 800 uliopewa kichwa “matumizi ya dawa za kuongeza nguvu mwilini nchini Ujerumani kuanzia mwaka wa 1950 hadi leo”.

Ripoti hiyo inadai kuwa baadhi ya wanasiasa wa wakati huo walijua kuhusu mpango huo na kuna shahidi mmoja aliyesema kuwa waziri mmoja wa mambo ya ndani ambaye hajatajwa jina lake alisema kuwa “wanariadha wao wa iliyokuwa Ujerumani ya magharibi walistahili kuwa na mazingira sawa ya kabla ya ushindani na wenzao wa mashariki.”

Huyu hapa waziri wa zamani wa mambo ya ndani Gerhard Groß anasema "Kile ambacho kimesababisha nchi nyingine kupata mafanikio katika mazoezi na mashindano ya kimataifa, kimewanyima wachezaji wetu fursa".

Ripoti hiyo haijachapishwa, lakini sehemu ya utafiti huo kuanzia mwaka wa 2012, imechapishwa na gazeti moja la Ujerumani suddeutsche zeitung ambalo lilifichua Jumamosi kuwa matumizi ya dawa hizo yalifanywa katika vitengo mbalimbali ikiwa ni pamoja na riadha na mpira wa miguu yaani kabumbu.

Waziri wa mambo ya ndani wa Ujerumani Christoph Bergner anasema matokeo ya mwisho yanastahili kupitiwa kabla ya kuchapishwa. Anasema "wizara ya mambo ya ndani ya Ujerumani haijapinga kufanya uchunguzi kuhusu suala hilo.

 Tumekuwa tukiunga mkono taasisi ya michezo na sayansi kwamba mahitaji ya kuzuia utoaji wa data lazima ulindwe.

No comments:

Post a Comment