KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, October 31, 2013

ROBINHO ASAFIRIA NYOTA YA COSTA AITWA NA SCOLARI

 Mshambuliaji wa AC Milan Robinho ameitwa na kocha Luiz Felipe Scolari kuelekea katika michezo miwili ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Honduras na Cile akichukua nafasi ya Diego Costa.
Mpiga mabao huyo wa Atletico Madrid ambaye hapo kabla alikuwa amejumuishwa lakini ikazuka utata mapema wiki hii baada ya kuitangazia dunia kuwa anataka kuitumikia Hispania Kimataifa licha ya mwaliko wa Scolari.
Lakini hata hivyo kocha huyo mwenye umri wa miaka 64 akaamua kubadili uchaguzi wake licha ya Costa kuwa katika kikubwa msimu huu.
Wakati hayo yakiwa hivyo mlinzi wa Paris Saint-Germain Thiago Silva amejumuishwa kikosini licha ya kuwa katika maumivu tangu mwezi Septemba huku mwenzake toka klabu moja Lucas Moura akiondolewa kutokana na kuwa hana nafasi katika timu yake.
 Pia mlinzi wa Corinthians Alexandre Pato, naye hayumo kikosini kwa kushindwa  kuonyesha uwezo katika michezo miwili dhidi ya  South Korea na Zambia mwezi Oktoba.
Mshambuliaji wa Chelsea Willian pia amejumuishwa na huenda akaichezea Selecao kwa mara ya kwanza.

Brazil itakuwa na michezo miwili dhidi ya Honduras mjini Miami Novemba 16, kabla ya kukutana na Chile mjini Toronto siku mbili baadaye.

No comments:

Post a Comment