KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, November 1, 2013

LIGI KUU TANZANIA BARA: AZAM NA MBEYA CITY NANI KUONGOZA LIGI KESHO?.


MSIMAMO WA LIGI  VPL 2013/2014
Rank
Teams
Played Wins Draw Lost GD Goal score Points
1 Yanga SC 12 7 4 1 17 28 25
2 Azam FC 11 6 5 0 10 17 23
3 Mbeya City 11 6 5 0 8 15 23
4 Simba SC 12 5 6 1 11 22 21
5 Kagera Sugar 12 4 5 3 3 13 17
6 Ruvu Shooting 11 4 4 3 3 13 16
7 Mtibwa Sugar 11 4 4 3 1 16 16
8 Coastal Union 11 3 6 2 4 10 15
9 JKT Ruvu 12 4 0 8 -7 9 12
10 Rhino Rangers 11 2 4 5 -6 9 10
11 Ashanti UTD 11 2 4 5 -9 10 10
12 Prisons FC 11 1 5 5 -9 6 8
13 JKT Oljoro 11 1 4 6 -8 8 7
14 Mgambo Shooting 11 1 2 8 -18 3 5

Raundi ya 12 ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) ambayo ipo katika raundi yake ya 12 inaendelea kesho (Novemba 2 mwaka huu) kwa mechi nne zitakazochezwa katika miji minne tofauti.

Mgambo Shooting na Coastal Union zitaoneshana kazi kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, Mbeya City na Ashanti United zitaumana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, Azam na Ruvu Shooting (Azam Complex, Dar es Salaam), na Mtibwa Sugar na Rhino Rangers (Uwanja wa Manungu, Morogoro).

Raundi hiyo itakamilika Novemba 3 mwaka huu kwa mechi moja ambapo Tanzania Prisons itakuwa mwenyeji wa Oljoro kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Mechi za kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo zitachezwa Novemba 6 na 7 mwaka huu. Novemba 6 ni JKT Ruvu vs Coastal Union, Ashanti United vs Simba, Kagera Sugar vs Mgambo Shooting, na Ruvu Shooting vs Mtibwa Sugar.

Novemba 7 mwaka huu, Azam itacheza na Mbeya City, Yanga itacheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Rhino itakuwa mwenyeji wa Tanzania Prisons.

No comments:

Post a Comment