Robin van Persie anasema ana imani kwamba meneja wa Manchester United
anayekabiliwa na shinikizo David Moyes atafanya vizuri Old Trafford.
Moyes amekumbana na mwanzo mbaya wa ufanyaji kazi wake ndani ya United kufuatia timu
hiyo kuwa katika matokeo mabaya katika juhudi zake za kutetea taji la Ligi ya Premia
pamoja ma kuharibu katika Kombe la FA raundi ya tatu.
United wako alama 11 nyuma ya viongozi wa msimamo wa ligi Arsenal na wanakabiliwa na
mlima katika juhudi zao za kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya msimu
ujao.
Kumekuwa na uvumi kwamba Moyes ameshindwa kupata imani kutoka kwa baadhi ya wachezaji wa United.
Na mahangaiko ya klabu hiyo katika juhudi zake za kudumisha viwango
vya nyakati za Alex, yamepelekea kushuka kwa thamani ya hisa za klabu
katika Soko la Hisa la New York.
Lakini straika wa United Van Persie, ambaye amekosa sehemu kubwa ya
msimu huu kutokana na jeraha la paja, ana imani kwamba Moyes atafanikiwa
akipewa muda.
“Ninafikiri kwamba anahitaji muda sawa na watu wengine wote, hasa
ukiwa mgeni katika klabu kubwa,” Van Persie aliambia gazeti la Guardian.
"Na kwa kweli, sidhani kwamba watu hawaelewi kwamba wanahitaji kumpa muda zaidi, na naongea kuhusu mashabiki na hata sisi.
“Atapata muda huo na kila mmoja anajua kwamba tutabadilisha mambo karibuni.
“Tulipoteza alama nyingi msimu huu, nyingi sana, lakini ikiwa
unataka kupigania mataji yote, ni lazima ucheze vyema na ushinde mechi
nyingi – lakini tunafanya kila tuwezalo kubadilisha hilo.
"Meneja ndiye kiongozi wetu katika hilo na anajaribu kadiri awezavyo na ninafikiri atabadilisha mambo.”
No comments:
Post a Comment