KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, January 17, 2014

Robin van Persie ampa nguvu Moyes kuhusu matokeo na kiwango cha United

Robin van Persie anasema ana imani kwamba meneja wa Manchester United anayekabiliwa na shinikizo David Moyes atafanya vizuri Old Trafford.
Moyes amekumbana na mwanzo mbaya wa ufanyaji kazi wake ndani ya United kufuatia timu hiyo kuwa katika matokeo mabaya katika juhudi zake za kutetea taji la Ligi ya Premia pamoja ma kuharibu katika Kombe la FA raundi ya tatu.
United wako alama 11 nyuma ya viongozi wa msimamo wa ligi Arsenal na wanakabiliwa na mlima katika juhudi zao za kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya msimu ujao.
Kumekuwa na uvumi kwamba Moyes ameshindwa kupata imani kutoka kwa baadhi ya wachezaji wa United.
Na mahangaiko ya klabu hiyo katika juhudi zake za kudumisha viwango vya nyakati za Alex, yamepelekea kushuka kwa thamani ya hisa za klabu katika Soko la Hisa la New York.
Lakini straika wa United Van Persie, ambaye amekosa sehemu kubwa ya msimu huu kutokana na jeraha la paja, ana imani kwamba Moyes atafanikiwa akipewa muda.
“Ninafikiri kwamba anahitaji muda sawa na watu wengine wote, hasa ukiwa mgeni katika klabu kubwa,” Van Persie aliambia gazeti la Guardian.
"Na kwa kweli, sidhani kwamba watu hawaelewi kwamba wanahitaji kumpa muda zaidi, na naongea kuhusu mashabiki na hata sisi.
“Atapata muda huo na kila mmoja anajua kwamba tutabadilisha mambo karibuni.
“Tulipoteza alama nyingi msimu huu, nyingi sana, lakini ikiwa unataka kupigania mataji yote, ni lazima ucheze vyema na ushinde mechi nyingi – lakini tunafanya kila tuwezalo kubadilisha hilo.
"Meneja ndiye kiongozi wetu katika hilo na anajaribu kadiri awezavyo na ninafikiri atabadilisha mambo.”

No comments:

Post a Comment