Mshambuliaji wa Misri, Gedo, amerejea katika klabu ya
Al Ahly, baada ya klabu ya ligi ya Uingereza ya Hull kusitisha huduma
za mchezaji huyo kwa klabu hiyo.
Gedo alikuwa anachezea Hull kwa mkopo.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 29,
alianza msimu wake wa pili na Hull mwezi Septemba baada ya kuingiza
mabao matano katika michezo 12 msimu uliopita.
Lakini hata hivyo amepata nafasi tu mara tatu tu na kutumiwa kama mchezaji wa akiba mara mbili katika ligi hiyo.
Wakati Hull ilipowasajili Nikica Jelavic na Shane Long ,hapo ndipo huduma za Gedo zilipositishwa Hull.
No comments:
Post a Comment