Coastal Union ya Tanga ‘Wagosi wa Kaya’ leo wametoka suluhu ya bila mabao dhidi ya Seeb SC inayoshiriki ligi kuu ya Oman.
Mchezo wa leo unakuwa ni mchezo wao wa nne tangu kuwasili nchini Oman Januari 9, kwa ziara
ya wiki mbili kujiandaa na ligi mzunguko wa pili Tanzania Bara.
Coastal Union, imeonyesha uhai katika kipindi cha pili
ambapo kipindi cha kwanza walishindwa kuonyesha makeke yao huku wachezaji
wa Seeb wakitumia zaidi sehemu ya kiungo, na kuwapa wakati mgumu Wagosi kushindwa kumiliki mpira.
Kipindi cha pili Seeb Club, walifanya mabadiliko kwa kutoa
wachezaji wawili wa ndani na mlinda mlango. Coastal Union waliendelea kucheza
bila kufanya mabadiliko.
Katika dakika za awali kipindi cha pili Seeb walionyesha
uhai na kulisumbua sana lango la Wagosi, lakini kufuli za Juma Nyoso na Othman
Tamim ziliendelea kuwa imara kuulinda mlango wa Shaaban Kado.
Aidha ilipofika dakika ya 76, kocha Yusuf Chipo alifanya
mabadiliko ya haraka haraka kwa kutoa wachezaji wanne na kuingiza wanne wengine zikiwa zimesalia dakika 15 mchezo kumalizika.
Alianza kutoka Othman Tamim akaingia Abdi Banda, baadae
akatoka Danny Lyanga akaingia Mohammed Miraji. Halafu zikiwa zimesalia dakika
chache mchezo kuisha alitoka Atupele Green akaingia Suleiman Kassim Selembe,
na kufanya mabadiliko ya mwisho kwa kumuingiza Abdullah Othman ‘Ustadh’ akatoka
Yayo Kato.
Listi ya leo ilikuwa: Shaaban Kado, Hamadi Juma, Othman
Tamim, Juma Said ‘Nyoso’, Mbwana Kibacha, Jerry Santo, Ally Nassor ‘Ufudu’, Danny
Lyanga, Atupele Green, Haruna Moshi ‘Boban’, na Yayo Kato.
Coastal Union tangu iwasili Oman imeshacheza mechi nne,
imeshinda mechi mbili kati ya Oman Club na Al Mussannah kwa mabao 2-0 kila
mechi. Halafu ikafungwa bao 1-0 na Fanja Club, leo imetoka suluhu ya bila
kufungana na Seeb Club.
COASTAL UNION
18 JANUARI, 2014
MUSCAT, OMAN
No comments:
Post a Comment